Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kaimu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam
(Dawasa) Romanus Mwang’ingo akielezea jambo mbele ya Waziri wa Maji na
Umwagiliaji Mhadisi Gerson Lwenge (wa pili kushoto) wakati wa ziara yake
ya kugagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ugawaji wa maji safi Dar es
Salaam na Pwani jana.
Waziri
wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akisikiliza maelezo
kutoka kwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji
Taka Dar es Salaam (Dawasa) Romanus Mwang’ingo kuhusu ujenzi wa tanki la
maji wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa
ugawaji wa maji safi Dar es Salaam na Pwani jana. Kulia ni Afisa
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Maji Safi Dar es Salaam (Dawasco) Mhandisi
Cyprian Luhemeja.
Waziri
wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akipewa maelezo na Meneja
Miradi wa Kampuni ya Wapcots Ltd Bw. P. G. Rajan kuhusu ujenzi wa tanki
la maji wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi
wa ugawaji wa maji safi Dar es Salaam na Pwani jana.
Baadhi
ya mafundi wakiwa wanalaza bomba la maji kama walivyokutwa na mpiga
picha wetu wakati wa ziara ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi
Gerson Lwenge kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ugawaji wa maji
safi Dar es Salaam na Pwani jana.
Seheme
ya hatua za ujenzi wa Matanki makubwa yenye uwezo wa kuhifadhi maji
ujazo wa lita milioni 6 kama katika maeneo ya Salasala na Bagamoyo .
Waziri
wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akiangalia mashine
inayotumiwa katika ujenzi na ulazaji wa mabomba ya maji alipotembelea
eneo la Kibamba na Hondogo ambapo ulazaji huo wa mabomba unaemndelea
ikiwa ni utekelezaji wa mradi mkubwa wa ugawaji wa maji safi Dar es
Salaam na Pwani.
Mkuu
wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Majjid Mwanga akielezea jambo mbele ya
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge (watatu kutoka
kushoto) wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa
ugawaji wa maji safi Dar es Salaam na Pwani jana. Kushoto kwa Waziri ni
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es
Salaam (Dawasa) Romanus Mwang’ingo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco
Mhandisi Cyprian Luhemeja (kushoto).
Waziri
Wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Jane Construction ambao ni
wakandarasi wa ujenzi wa mradi wa ugawaji maji safi Dar es Salaam na
Pwani mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kukagua mradi huo jana.
Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO
…………………………………………………………………………
Na: Frank Shija – MAELEZO
Mkandarasi
anayejenga mradi wa ujenzi wa miundombinu ya ugawaji maji Dar es Salaam
na Pwani atakiwa kukamilisha mradi huo kwa wakati kulingana na
makubaliano yaliyopo ndani ya mkataba.
Agizo
hilo limetolewa jana na Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson
Lwenge wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo
ambapo alitembelea kazi ya ulazaji wa mabomba katika eneo la Kibamba na
Hondogo, Kituo cha kusukuma maji Makongo Juu, ujenzi wa matanki ya maji
maeneo ya Changanyikeni, Mabwepande na Bagamoyo.
“
Nimeona mkandarasi sasa hivi anaenda vizuri, na niseme tu kazi hii
ikamilike kama kama ilivyo katika mkataba sitaongeza muda, hivyo ifikapo
tarehe 16, Novemba 2017 mradi huu uwe umekamilika” alisema Mhandisi
Lwenge.
Mhandisi
Lwenge amesema kuwa mradi huu ni muendelezo wa kuhakikisha wananchi
wanapatiwa huduma ambapo watu zaidi ya wakazi laki tano wa maeneo ya
Jiji la Dar es Salaam na Pwani watanufaika baada ya mradi huu
kukamilika.
Mhandisi
Lwenge amesema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha Wananchi wake
wanaondokana na adha ya ukosefu wa huduma ya maji katika maeneo
wanayoishi ili waweze kujikitika katika kufanya kazi.
Aidha
Mhandisi Lwenge aalisema kuwa ameridhishwa na kasi ya maendeleo ya
ujenzi wa mradi huo na kumtaka Mkandarasi wa mradi huo kuhakikisha
mradi huo unakamilika ifikapo tarehe 16 Novemba mwezi 2017 kama ilivyo
katika makubaliano.
Awali
akitoa maelezo ya mradi huo, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji
Safi na Maji Taka Dar es Salaam (Dawasa) Mhadisi Romanus Mwang’ingo
amesema kuwa Mradi wa Usambazaji wa Maji Safi Dar es Salaam na Pwani
unahusisha ujenzi wa matenki tisa (9) ya kusambaza na kuhifadhi maji
yenye ukubwa wa kuhifadhi lita milioni 3 hadi 6, ujenzi wa vituo vinne
(4) vya kusukuma maji, ununuzi na ufungaji wa Pampu kubwa za kusukuma
maji 16, ununuzi wa transfoma na ufungaji njia za umeme wa msongo
mkubwa, ununuzi na ulazaji wa mabomba makubwa ya ugawaji maji na ulazaji
maji wa mabomba ya usambazaji maji mtaani yatakayokuwa na urefu wa
jumla ya kilometa zipatazo 477.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Majjid Mwanga ameipongeza
Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (Dawasa) kwa jitihada
zake za kutatua changamoto za upatikanaji wa maji safi kwa wananchi wa
wilaya yake.
“
Kipekee kabisa kwa niaba ya wananchi wa Bagamoyo niseme tu mradi huu wa
tenki la ujazo wa lita 6Milioni changamoto ya maji itabaki kuwa
historia kwani tutaachana na utumiaji wa miundombinu ya zamani” alisema
Majjid.
Naye
Mhandisi Mkazi wa Kampuni ya Jane Construction ambao ndiyo mkandaarasi
mkuu wa mradi huo Bw. Ashish Srivagtava amemshukuru Waziri kwa
kutembelea na kujiongena mradi huo na kuahidi kuwa mradi huo utakamilika
kwa wakati kama ambavyo Waziri ameelekeza.
Katika
ziara hiyo ya kukagua mradi wa usambazaji maji safi Dar es Salaam na
Pwani waziri alitembelea kazi ya ulazaji wa mabomba katika eneo la
Kibamba na Hondogo, Kituo cha kusukuma maji Makongo Juu, ujenzi wa
matanki ya maji maeneo ya Changanyikeni, Mabwepande na Bagamoyo.
Maeneo
yatakayo nufaika na mradi huu ni pamoja na Salasala, Bunju, Wazo,
Makongo, Changanyikeni, Bagamoyo, Mpiji, Zinga, Kitope, Ukuni, Kerenge,
Buma, Mataya na ukanda maalum wa EPZA ambayo ni maeneo yanayo hudumiwa
na mtambo wa Ruvu chini. Ambayo ni maeneo mengine yatakayo nufaika na
mradi huu ni yale yaliyopo kati ya Mbezi luisi na kiluvya, ambayo ni
Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Msakuzi, Makabe, Malamba mawili na Msigani.
Maeneo haya huhudumiwa na mtambo wa ruvu juu ambao ulizinduliwa na
mh,Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Juni 21,2017.
Mradi
wa usambazaji wa maji safi Dar es Salaam na Pwani unatekelezwa na
Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasa) ulianza tangu mwezi Machi
2016 na unatarajiwa kukamilika tarehe 16, Novemba, 2017 unathamani ya
shilingi bilioni 72 ambazo ni mkopo nafuu kutoka India, nchi mshirika wa
maendeleo.
0 comments:
Post a Comment