Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mbunge wa Jimbo la Temeke Abdalla Mtolea akiwa na Meg Munn kutoka taasisi ya Global Patber kutoka Nchini Uingerza na kutembelea kata ya Mtoni katika Kikundi cha Mfendengeni wanaojishughulisha na shughuli za upandaji wa vitalu vya miti ikiwa ni katika mradi unaosimamiwa na ofisi ya Mbunge.
Mbunge wa Jimbo la Temeke Abdalla Mtolea akiwa na Meg Munn kutoka taasisi ya Global Patber kutoka Nchini Uingerza na kutembelea kata ya Azimio katika kikundi cha Saccos ya Vijana kinachojishughulisha na mradi wa utotoleshaji wa mayai ya kuku.
Mbunge wa Jimbo la Temeke Abdalla Mtolea akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa Mtongani Unguja Kata ya Azimio akishuhudiwa na Mweyekiti wa Mtaa huo Zainab Liganja wakati wa ziara ya Mbunge huyo katika Miradi mbalimbali ya kimaendeleo katika kata saba za Wilaya ya Temeke.
Mbunge
wa Jimbo la Temeke Abdalla Mtolea amevipongeza vikundi saba
vilivyoiwezeshwa na Mfuko wa Mbunge kwa kuweza kujiendeleza na kuanza
kufikia malengo waliyojiwekea.
Aliyasema
hayo katika ziara ya vikundi saba katika kata nne za Wilaya ya Temeke
akiwa ameongoza na wawakilishi kutoka Taasisi ya Global Patner ya nchini
Uingereza.
Katika
kata nne alizotembelea, Mtolea amewaonyesha wageni hao namna wananchi
wanavyojikita katika kujiiunua kiuchumi kwa kuunda vikundi vyao binafsi
na kujishughulisha na shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo ufugaji wa
kuku wa mayai, kutotoa mayai, upandaji na uuzaji wa miti aina
mbalimbali, na sanaa za mikono kama batiki, vikoba na masuala ya sanaa
ya uigizaji.
Mtolea allitembelea kata ya Mtoni, Azimio, Vituka, Makangarawe na Kilakala
0 comments:
Post a Comment