Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MUHIMBILI YAADHIMISHA SIKU YA WAKUNGA DUNIANI KWA KUPIMA AFYA WANANCHI LEO

MUHIMBILI YAADHIMISHA SIKU YA WAKUNGA DUNIANI KWA KUPIMA AFYA WANANCHI LEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mgeni rasmi, Flora Kimaro ambaye ni Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi Taasisi ya MOI akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wakunga Duniani yaliofanyika Tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili leo. Pamoja na maadhimisho hayo Chama cha Wakunga Nchini (TAMA) kimepongezwa kwa kutoa huduma za afya ambapo watu wanapima afya leo katika hospitali hiyo. Siku ya Wakunga Duniani huadhimishwa Mei 5, kila mwaka, lakini TAMA tawi la Muhimbili imeamua kuadhimisha siku hii katika wiki ya unyonyeshaji duniani.

Baadhi ya wananchi waliofika katika siku ya maadhimisho hayo wakimsikiliza mgeni rasmi,
Mgeni rasmi akikakata utepe akiashiria kuanza kwa shughuli za maadhimisho hayo ikiwa ni pamoja na kupima watu mbalimbali afya
Mmoja wa wauguzi, Gladisia Kessy akimpima afya mmoja wa watu waliofika Muhimbili leo kwa ajili ya kushuhudia maadhimisho hayo.
Mgeni rasmi pamoja na baadhi ya maofisa wa Muhimbili wakiwamo wakunga wakielekea meza kuu leo.
Baadhi ya watu wakifuatilia maadhimisho hay oleo.
Maofisa wa Muhimbili wakiwamo wakunga wakiwa katika picha pamoja leo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa