Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa Ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa
Na Agness Moshi – MAELEZO.
Ni
jambo la kawaida katika miaka hii kuona takwimu za tafiti mbalimbali
zikitolewa na Taasisi , Serikali , Mashirika au baadhi ya watu kwenye
vyombo vya habari au mitandao ya kijamii ambayo kwa sasa imejizolea
umarafu kutokana ongezeko la watumiaji wake Nchini.
Takwimu
hizo zimekua zikitolewa kwa lengo la kutoa taarifa, kuelimisha au
kusaidia katika kupanga mipango mbalimbali kwa maendeleo ya Taasisi,
Shirika husika au Nchi kwa ujumla . Wakati mwingine zimekua zikiibua
hisia za wananchi kutaka kujua zaidi kuhusiana na taarifa hizo hivyo
kupelekea vyombo vya habari kufuatilia taarifa hizo kwa undani.
Si
jambo la ajabu kuona taarifa za takwimu kwenye magazeti, televisheni,
mitandao ya kijamii au kuzisikia kwenye redio. Mtakua mashahidi wangu
kwenye hili. Lakini je, takwimu hizi tunazozisikia na kuziona zinafuata
Sheria na taratibu za utoji takwimu?
Ni
wazi kila kitu kina utaratibu na sheria zake, vivyo hivyo utoaji
takwimu una sheria na taratibu zake kuanzia ukusanyaji data hadi
uwasilishwaji wake kwa jamii au taasisi husika.
Uwepo
wa taratibu za utoaji taarifa za takwimu umethibitishwa na Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa Ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alipokua
akiongea na waadishi wa Habari Jijini Dar es Salaam mapema wiki hii,
kufuatia taarifa zisizo sahihi zilizotolewa na Kampuni ya Utafiti ya
Geopoll yenye Ofisi ya Kanda Ya Afrika, mjini Nairobi, Kenya kuhusiana
na viwango vya idadi ya watazamaji wa vituo vya habari hapa nchini.
“Taarifa
zozote zinazohusu utafiti ni lazima zizingatie vigezo vyote
vinavyotakiwa na vilivyoidhinishwa na mamlaka inayotambulika
kisheria”,alisema Dkt.Chuwa.
Alivitaja
baadhi ya vigezo hivyo ambavyo ni uwazi na ukweli, uhusishwaji wa
wahusika na wadau mbalimbali , ushirikishwaji wa mamlaka husika na
kuzingatiwa kwa weledi.
“Takwimu
zinazotolewa bila kuzingatia taratibu zinazohitajika hazitatambulika na
Serikali kwani utoaji wa Takwimu haufanywi kama unavyohesabu migomba
shambani, ni lazima wahusika wafuate taratibu zote”, alifafanua
Dkt.Chuwa.
Dkt.
Chuwa amesisitiza kuwa, ni vyema Taasisi yoyote inayotaka kukusanya
taarifa zozote za takwimu kuhakikisha wanashirikisha wahusika ili
kuepusha mkanganyiko na upotoshwaji kama ilivyofanywa na Kampuni hiyo
kutoka Nairobi, Kenya. Aliendelea
kwa kusema, Serikali haitatambua Takwimu zitakazotolewa bila kufuta
sheria ya takwimu na kukidhi vigezo rasmi kwani zinaweza kuwa chanzo cha
maafa.
“Takwimu si kitu cha masihara, takwimu ni vita” aliongeza Dkt.Chuwa.
Kufuatia
kuathiriwa kwa mahusiano ya kiutendaji baina ya vyombo vya habari hapa
nchini yaliyosababishwa na taarifa iliyotolewa na kampuni ya Geopoll
hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii.
Ofisi
ya Takwimu nchini inapenda kuzijulisha Taasisi zinazojihusisha na
utoaji wa taarifa zinazotokana na utafiti kuwa, Sheria ya takwimu ya
mwaka 2015 kifungu cha 6 imeipa NBS mamlaka ya kutoa, kusimamia na
kuratibu upatikanaji wa takwimu rasmi kwa ajili ya matumizi ya Serikali
na Wadau wa Takwimu.
“Hapo
awali Ofisi ya Taifa ya Takwimu haikua na meno lakini mara baada ya
marekebisho ya Sheria hiyo, sasa inayo meno ya kuiwezesha kudhibiti
utoaji holea wa Takwimu nchini” Alisema Dkt. Chuwa.
Dkt.Chuwa
ametoa rai kwa watoa takwimu kufuta kanuni na taratibu kama watashindwa
hawana budi kuacha mara moja kwani shughuli ya utoaji takwimu si
lelemama kama inavyodhaniwa.
Naye,
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa
amewataka Waandishi wa Habari kuacha kuandika taarifa za takwimu ambazo
hazijahazijathibitishwa na kutambulika na NBS,pia zisizo na mashiko
kwa Wananchi na Serikali kwa ujumla.
“Vyombo
vya habari nchini viache kushabikia taarifa zinazotolewa na Taasisi
zozote zisizo tambulika na kuthibitishwa na NBS hususani katika maswala
ya Takwimu”, alisisitiza Bi. Zamaradi.
Wahenga
walisema “Mchelea mwana kulia hulia mwenyewe” wakimaanisha mzazi
anapozembea kulea mtoto wake baadae anapoharibikiwa inakua hasara
kwake.Hivyo basi, NBS imefanya jambo jema kukemea watoa takwimu
wasiofuata sheria ili kuepusha madhara yoyote yanayoweza kusababishwa na
takwimu zisizo rasmi.
Kwa
watumiaji wa mitandao ya kijamii, ni vyema kutoamini na kujiepusha na
usambazaji wa taarifa ambazo hazina uhakika kwasababu wanaweza kuwa
chanzo cha uvunjifu wa Amani ambayo ndio
0 comments:
Post a Comment