Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » NBS YAWATAKA WATOA TAKWIMU WANGATIE TARATIBU KUEPUSHA UPOTOSHAJI

NBS YAWATAKA WATOA TAKWIMU WANGATIE TARATIBU KUEPUSHA UPOTOSHAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa Ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa 

Na Agness Moshi – MAELEZO.
Ni jambo la kawaida katika miaka hii kuona takwimu za tafiti mbalimbali zikitolewa na Taasisi , Serikali , Mashirika  au baadhi ya watu kwenye vyombo vya habari au mitandao ya kijamii ambayo kwa sasa imejizolea umarafu  kutokana  ongezeko la watumiaji wake Nchini.
Takwimu hizo zimekua zikitolewa kwa lengo la kutoa taarifa, kuelimisha au kusaidia katika kupanga mipango mbalimbali kwa maendeleo ya Taasisi, Shirika  husika au Nchi kwa ujumla . Wakati mwingine zimekua zikiibua hisia za wananchi kutaka kujua zaidi kuhusiana na taarifa hizo hivyo kupelekea vyombo vya habari kufuatilia taarifa hizo kwa undani.
Si jambo la ajabu kuona taarifa za takwimu kwenye magazeti, televisheni, mitandao ya kijamii au kuzisikia kwenye redio. Mtakua mashahidi wangu kwenye hili. Lakini je, takwimu hizi tunazozisikia na kuziona zinafuata Sheria na taratibu za utoji takwimu?
Ni wazi kila kitu kina utaratibu na sheria zake, vivyo hivyo utoaji takwimu una sheria na taratibu zake kuanzia ukusanyaji data hadi uwasilishwaji wake kwa jamii au taasisi husika.
Uwepo wa taratibu za utoaji taarifa za takwimu umethibitishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa Ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alipokua akiongea na waadishi wa Habari Jijini Dar es Salaam mapema wiki hii, kufuatia taarifa zisizo sahihi zilizotolewa na Kampuni ya Utafiti ya Geopoll yenye Ofisi ya Kanda Ya Afrika, mjini Nairobi, Kenya kuhusiana na viwango  vya idadi ya watazamaji wa vituo vya habari hapa nchini.
“Taarifa zozote zinazohusu utafiti ni lazima zizingatie vigezo vyote vinavyotakiwa na vilivyoidhinishwa na mamlaka inayotambulika kisheria”,alisema Dkt.Chuwa.
Alivitaja baadhi ya vigezo hivyo ambavyo ni uwazi na ukweli, uhusishwaji wa wahusika na wadau mbalimbali , ushirikishwaji wa mamlaka husika na  kuzingatiwa kwa weledi.
“Takwimu zinazotolewa bila kuzingatia taratibu zinazohitajika hazitatambulika na Serikali kwani utoaji wa Takwimu haufanywi kama unavyohesabu migomba shambani, ni lazima wahusika wafuate taratibu zote”, alifafanua Dkt.Chuwa.
 Dkt. Chuwa amesisitiza kuwa, ni vyema Taasisi yoyote inayotaka kukusanya taarifa zozote za takwimu kuhakikisha wanashirikisha wahusika ili kuepusha mkanganyiko na upotoshwaji kama ilivyofanywa na Kampuni hiyo kutoka Nairobi, Kenya. Aliendelea kwa kusema, Serikali haitatambua Takwimu zitakazotolewa bila kufuta sheria ya takwimu na kukidhi vigezo rasmi kwani zinaweza kuwa chanzo cha maafa.
“Takwimu si kitu cha masihara, takwimu ni vita” aliongeza Dkt.Chuwa.
 Kufuatia kuathiriwa kwa mahusiano ya kiutendaji baina ya vyombo vya habari hapa nchini yaliyosababishwa na taarifa iliyotolewa na kampuni ya Geopoll hivi karibuni kupitia mitandao ya kijamii.
 Ofisi ya Takwimu nchini inapenda kuzijulisha Taasisi zinazojihusisha na utoaji wa taarifa zinazotokana na utafiti kuwa, Sheria ya takwimu ya mwaka 2015 kifungu  cha 6  imeipa NBS mamlaka ya kutoa, kusimamia na kuratibu upatikanaji wa takwimu  rasmi kwa ajili ya matumizi ya Serikali na Wadau wa Takwimu.
 “Hapo awali Ofisi ya Taifa ya Takwimu haikua na meno lakini mara baada ya marekebisho ya Sheria hiyo, sasa inayo meno ya kuiwezesha kudhibiti utoaji holea wa Takwimu nchini” Alisema Dkt. Chuwa.
Dkt.Chuwa ametoa rai kwa watoa takwimu kufuta kanuni na taratibu kama watashindwa hawana budi kuacha mara moja kwani shughuli ya utoaji takwimu si lelemama kama inavyodhaniwa.
Naye, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa amewataka Waandishi wa Habari kuacha kuandika taarifa  za takwimu ambazo  hazijahazijathibitishwa na  kutambulika  na NBS,pia zisizo na mashiko kwa Wananchi na Serikali kwa ujumla.
“Vyombo vya habari nchini viache kushabikia taarifa zinazotolewa na Taasisi zozote zisizo tambulika na kuthibitishwa na NBS hususani katika maswala ya Takwimu”, alisisitiza Bi. Zamaradi.
Wahenga walisema “Mchelea mwana kulia hulia mwenyewe” wakimaanisha mzazi anapozembea kulea mtoto wake baadae anapoharibikiwa inakua hasara kwake.Hivyo basi, NBS imefanya jambo jema kukemea watoa takwimu wasiofuata sheria ili kuepusha madhara yoyote yanayoweza kusababishwa na takwimu zisizo rasmi.
Kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, ni vyema  kutoamini na kujiepusha na usambazaji wa taarifa ambazo hazina uhakika  kwasababu wanaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa Amani ambayo ndio



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa