Na. Aron Msigwa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu Wenye Ulemavu
Mhe. Jenista Mhagama ameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa
kuendelea kusimamia matumizi bora ya rasilimali inazopewa na Serikali na
kuzitaka taasisi nyingine za Serikali kuiga mfano huo.
Mhe.
Muhagama ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam mara baada ya
kutembelea ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuangalia utekelezaji
wa maagizo ya Bunge kupitia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria
na Utawala Bora iliyoridhia Bunge lipitishe fedha kiasi cha shilingi
bilioni 10 kuiwezesha Tume kufanya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari
la Kudumu la Wapiga Kura nchini .
Akizungumza
na watendaji na baadhi ya watumishi wa Tume amesema kuwa ameridhishwa
na utendaji kazi wao na namna Tume ilivyojipanga
kutekeleza jukumu la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
kuelekea uchaguzi ujao wa mwaka 2020 kwa kuwa na mpango Kazi,
unaochambua na kubainisha mahitaji muhimu yanayotakiwa, lini na wapi ili
kazi hiyo iweze kufanyika kwa umakini.
“
Naipongeza sana Tume kwa kuendelea kufanya vizuri , nimegundua kuwa
imejipanga vizuri kutekeleza majukumu yake ambayo yameainishwa
Katika Katiba, kwa niaba ya Waziri Mkuu nimekuja hapa na timu ya
watendaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kuangalia utekelezaji wa maagizo
ya Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala Bora walioridhia Bunge
lipitishe fedha shilingi Bilioni 10 ili kuiwezesha
kufanya maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura”
Amesema.
Mhe.
Mhagama ameeleza kuwa kazi hiyo kazi ya utekelezaji wa maagizo hayo ya
Bunge inazingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 5 kifungu kidogo cha 3 (a) ambacho
kimeweka uanzishwaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura nchini na Ibara
ya 74 kifungu kidogo cha 6 (a) na (e) ambacho kinaipa Tume madaraka ya
kuchukua jukumu la kuandikisha wapiga Kura nchini
Tanzania.
Aidha,
ameongeza kuwa Sheria ya Uchaguzi kifungu cha 15 (3) kinaipa madaraka
Tume ya Uchaguzi kutengeneza mfumo na utaratibu wa
uandikishaji wa wapiga Kura nchini na uboreshaji wa daftari hilo mara
mbili kati ya Uchaguzi mkuu mmoja na unaofuata.
“Tunaelekea
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 kwa hiyo ili tuzingatie takwa la Katiba na
takwa la Sheria ya Uchaguzi ambayo inasimamiwa
na Tume ni lazima sasa Serikali ione kwamba inaisaidia Tume ya Taifa ya
Uchaguzi na wote tunajua kuwa utendaji wake ni huru lakini Serikali
tunaowajibu wa kuhakikisha kuwa Tume inafanya kazi yake vizuri”
Amesisitiza.
Kwa
Upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge),
Maimuna Tarishi akizungumza mara baada ya kumalizika kwa
ziara hiyo ameipongeza uongozi wa Tume kwa kuonyesha mfano katika
kuondoa mazoea katika utendaji kazi ikiwemo utunzaji wa mali na
rasilimali za Serikali.
Amesema kuwa Serikali itaendelea kuijengea uwezo Tume kwa kuipatia rasilimali na vitendea kazi inavyohitaji ili iweze kutimiza
majukumu yake kwa wakati.
Naye
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima
Ramadhani akizungumza mara baada ya kumalizika kwa ziara hiyo
amemshukuru viongozi hao kwa kuzitembelea ofisi za Tume kuangalia
maandalizi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na
kuishukuru Serikali kwa kutenga shilingi Bilioni 10 zitakazotumika kwa
ajili ya uboreshaji huo.
Amesisitiza
kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi imejipanga kulitekeleza jukumu hilo
kikamilifu na inaendelea kufanya maandalizi mbalimbali
yakiwemo ya kuzipitia Mashine za BVR zitakazotumika kuandikisha wapiga
Kura , kupitia mifumo Sheria na kanuni za Uboreshaji, kupitia vifaa
vilivyopo ili kupunguza mzigo wa kununua vifaa vipya wakati wa zoezi
hilo.
0 comments:
Post a Comment