Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Agness Moshi
Kampuni
ya kurusha matangazo kwa njia ya digitali na waauzaji wa ving’amuzi
Startimes na Shirika la utangazaji la Sibuka waidhamini ligi ya mpira wa
kikapu Dar es Salaam (RBA).
Hayo yamesemwa na Afisa Mahusiano wa
Startimes Bw. Samuel Gisayi wakati akitambulishwa na Chama Cha Mpira wa
Kikapu (BD) kwa waandishi wa habari kuwa mdhamini mpya wa RBA,
Jijini Dar es Salaam.
Bw. Gisayi amesema kuwa udhamini kwa ligi
hiyo kwa sasa ni wa muda mfupi, na baada ya kumalizika kwa ligi ya RBA
wako kwenye mazungumzo ya kuwa wadhamini wa mojakwa moja wa mchezo huo
kwa kipindi cha miaka mitano.
“Tumeamua kudhamini RBA ili kukuza
vipaji vya wacheza mpira wa kikapu kwa sababu Makampuni mengi yamekua
yakiwekeza kwenye mpira wa miguu na kusahau mchezo huu kusaidia
wachezaji waweze kuonekana na kusajiliwa kwenye timu kubwa” , alisema
Bw.Gisayi.
Bw.Gisayi ameongeza kuwa tayari wamefanya mambo
mbalimbali ili kuweza kufanikisha mashindano hayo ikiwemo kuboresha
viwanja ambavyo mchezo huo utafanyika na kudhamini gharama zote za
uendeshaji wa ligi hiyo kuanzia mzunguko wapili mpaka fainali.
“Ukiachana
na uuzaji wa ving’amuzi Startimes inashirikiana na Jamii katika kuleta
maendeleo kwenye sekta mbalimbali ikiwemo michezo ili kuinua vipaji vya
Watanzania” ,alisititiza Bw.Gisayi.
Bw.Gisayi ametoa wito kwa
wafanyabiashara kupeleka matangazo yao kwenye vituo vyao ili waweze
kutangaziwa kwa bei rahisi wakati wa ligi hiyo , pia ametaka wadau
mbalimbali kutoa ushirikiano kwa mchezo wa mpira wa kikapu kama michezo
mingine .
Kwa upande wake Mkurugenzi wa habari na Mawasiliano
Bw.Peter Mpangala amesema kuwa wanaimani mchezo huo utafika mbali na
utakua wa kibiashara kupitia udhamini wa startimes na sibuka kwasababu
wamepata kupata fursa ya kuwa na kurusha michezo yao mubashara kwenye
televisheni.
“Ukiwa na kipindi kwenye televisheni unakaribisha
wadau wengi zaidi kuudhamini mchezo na tunategemea biashara kubwa kwa
wachezaji”, alisema Bw.Mpangala.
Bw.Mpangala ameongeza kuwa
amefurahishwa na kitendo cha startimes kuwadhamini kwa sababu kupitia
kampuni hiyo ambayo inashirikiana na taasisi ya kubwa inayosimamia
mchezo huo Duniani (FIBA) wataweza kufikia malengo ya kuufikisha mchezo
huo mbali.
Naye ,Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa
wa Dar es Salaam Bw.Okare Emesu amesema kuwa, wana mikakati ya pamoja
na wadhamini hao ili kuufanya mchezo huo uwe wa kibiashara na uweze
kufika mbele zaidi, vilevile ametoa wito kwa wananchi kufuatilia vipindi
vya mchezo huo vitavyoonyeshwa kwenye king’amuzi cha startimes kupitia
Tv Sibuka kila siku ya Ijumaa, Jumamosi na Jumapili saa kumi na mbili
jioni.
Ligi ya RBA kwa sasa ipo kwenye mzunguko wa pili na
baada ya wiki 3 hatua ya mtoano (playoff) itaanza rasmi kuelekea
fainali itakayofanyika tarehe 24 mwezi huu Uwanja wa Taifa .
0 comments:
Post a Comment