Mkurugenzi
Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bi. Lilian Liundi
akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari
waliokutanishwa ili kujadili namna ya kufanya kazi katika Tamasha
la 14 la Kijinsia litakalofanyika Septemba 5 hadi 8 mwaka huu katika
Ofisi za Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) Mabibo jijini Dar es
salaam.
Balozi Getrude Mongella akizungumza na waandishi pamoja na wahariri wa vyombo vya habari leo kuhusu maandalizi ya Tamasha
la 14 la Kijinsia litakalofanyika Septemba 5 hadi 8 mwaka huu katika
Ofisi za Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) Mabibo jijini Dar es
salaam.
Afisa
Program uchambuzi na Machapisho kutoka TGNP Mtandao, Bw. Deogratius
Temba akizungumza jambo wakati wa semina iliyowakutanisha waandishi wa
habari pamoja na wahariri wa vyombo mbalimbali iliondaliwa na Mtandao TGNP .
Baadhi ya wahariri pamoja na wafanyakazi wa Mtandao TGNP wakiwa kwenye semina
Afisa
Habari wa TGNP ,Monica John akizungumza na wahariri wa vyombo
vya habari waliofika kwenye semina iliyokuwa inahusu tamasha la wanawake
litakalofanyika jijini Dar mwaka huu.
Baadhi
ya wahariri wa vyombo vya habari wakichangia mada kwenye semina
iliyowakutanisha ili kujadili namna nzuri ya kufanya kazi katika Tamasha
la 14 la Kijinsia litakalofanyika Septemba 5 hadi 8 mwaka huu katika
Ofisi za Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) Mabibo jijini Dar es
salaam.
Picha ya Pamoja
TGNP
Mtandao kutambua mchongo wa wanawake walioshiriki kuleta maendelea
nchini hapa nchini Tanzania katika Tamasha la 14 la Kijinsia
litakalofanyika Septemba 5 hadi 8 mwaka huu katika Ofisi za Mtandao wa
Jinsia Tanzania (TGNP) Mabibo jijini Dar es salaam.
Akizungumza
na katika semina ya kutoa elimu juu ya tamasha hilo kwa Wahariri wa
vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP,
Lilian Lihundi, alisema lengo la tamasha hilo ni kusherehekea, kujadili
changamoto na mafanikio ya harakati wanazozifanya.
Alisema
Tamasha hilo litawahusisha wanawake mbalimbali ambao wamepata mafanikio
makubwa katika harataki za ukombozi wa mwanamke na kuhakikisha usawa wa
kijinsia.
“Katika
siku zote nne wanawake zaidi ya 1000 watakaa na kujadili changamoto
zinazoikumba jamii, kusherekea mafanikio yaliyopatikana na kujenga
nguvu ya pamoja katika kuhakikisha ukatili wa kijinsia unaisha.
“Kutokana
na kauli mbiu ya tamasha hili inavyosema kuwa Mageuzi ya Mfumo
Kandamizi kwa Usawa wa Kijinsia na Maendeleo. Tunakata kuangalia
mwanamke anaonekana vipi katika hazma ya Serikali kuifanya Tanzania kuwa
ya viwanda,” alisema Lilian.
Aidha
alisema wajasilimali wataonesha bidhaa na kupata elimu ya namna gani
wanaweza kuboresha bidhaa zao na ufungashaji ili waweze kuingia kwenye
soko la ushindani la bidhaa za ndani na nje ya nchi kutoka Shirika la
Viwanda vidogo (Sido), Mamlaka ya Chakula a Dawa (TFDA) na Taasisi ya
Udhibiti Ubora (TBS) kwa ajili ya kupewa.
0 comments:
Post a Comment