Afisa Matukio wa Airtel Tanzania akikabidhi simu maalum zitakazotumika kuendesha mradi wa VSOMO kwa Msajili Mkuu Veta Kipawa(Registry), Bw, Harold Mganga, (kushoto), akishuhudiwa na Mratibu
wa Miradi na Kozi fupi. (Project and Short Course Coordinator)Veta
Kipawa Gosbert Kakiziba (katikati) simu hizo zimetolewa kwa kwaajili
ya mradi wa VSOMO. VSOMO ni applikesheni maalum inayotoa mafunzo ya
ufundi stadi ya VETA kwa njia ya mtandao inayodhaminiwa na Airtel
Tanzania.
Afisa Matukio wa Airtel Dangio Kaniki (kulia) akimuonyesha applikesheni ya VSOMO Mkuu wa Usajili Veta Kipawa (Registry) Bw, Harold Mganga (katikati) pamoja na Mratibu wa Miradi na Kozi fupi. (Project and Short Course Coordinator) Veta Kipaw bw, Gosbert
Kakiziba (kulia). hafla fupi ya makabidhiano ya simu hizo
yaliyofanyika Veta Kipawa. Aplikesheni ya VSOMO inatoa mafunzo ya
ufundi stadi ya VETA kwa njia ya mtandao inayodhaminiwa na Airtel
Tanzania.
Mamlaka
ya elimu ya ufundi Tanzania (VETA) kwa kupitia mfumo wa mafunzo kwa
mtandao wa VSOMO unaodhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imebainisha
kuwa iko tayari kuhudumia vikundi au jamii ya wanaotaka kujifunza
ufundi stadi kwa kupeleka timu yao ya mafunzo kwa vitendo popote ili
kuhakikisha dhana ya uchumi wa viwanda inakamilika kwa kuwa na mafundi
wazuri waliohitimu ufundi katika chuo maalumu nchini
Hayo
yamebainishwa na mkuu wa chuo cha veta kipawa ambae pia ni msimamizi wa
mradi wa mafunzo kwa njia ya simu unaodhaminiwa a Airtel kwa lengo la
kutoa FURSA kwa vijana wegi mjini kupata ujuzi na kujiajiri Mhandisi
Lucius Luteganya
VETA
tuko tayari kuwafuata wanafunzi wetu endapo watajiandikisha na
kuhamasihana kwa kikundi kusoma kwa njia ya mtandao wa VSOMO , ikiwa
watakuwa vijana kuanzia 15-20 na wakipenda kupata mafunzo waliko basi
sisi tutawafuata waliko ili kuhakikisha wanahudumiwa na mobile trainers wetu”
“sasa
hivi kupitia mtandao wa Vsomo tunakozi 12, wanafunzi wanaweza
wakajisomea wawapo popote mara baada ya kupakua App yetu ya VSOMO na
kulipia kozi anayotaka” alisisitiza Luteganya
Eng
Luteganja alitaja kozi hizo kuwa ni “Tunampango waongeza kozi zingine
15 hivi karibuni lakini kwa sasa zilizopo tayari kwenye mtandao ni
Huduma ya chakula na mbinu za kuhudumia wateja, Matengenezo ya kompyuta,
umeme wa viwandani, ufundi Bomba wa Majumbani , Umeme wa magari, Ufundi
umeme wa manyumbani, Ufundi pikipiki, Ufundi wa simu za mkononi, Ufundi
Alluminium, Utaalamu wa maswala ya urembo pamoja ma Ufundi wa kuchomea
vyuma.
Tangu
VETA na Airtel walipozindua mfumo huu wa mafunzo kwa njia ya mtandao
waVSOMO mwezi wa Juni 2016 Mfumo huu wa VSOMO sasani umepata umaarufu
mkubwa kwa vijana ambapo takwimu zinaonyesha zaidi ya vijana 30,000
tayari wamepakua application ya VSOMO, 8000 wamejiandikisha na kati yao
50 wameshasoma kozi mbalimbali na kupata vyeti vyao vya ufundi stadi
kutoka VETA.
kujiandikisha
katika mojawapo ya kozi 12 zinazopatikana katika application ya VSOMO
mwanafunzi atalipia kwa simu yake gharama ndogo ya shilingi 120,000 tu
kupitia huduma ya Airtel Money kwa kupiga *150*60#. na kufanya malipo
ambazo gharama hizi zitamuwezesha kuja kupata mafunzo kwa vitendo bila
malipo ya ziada.
0 comments:
Post a Comment