Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WANAOTAPELI KWA JINA LA MAMA SALMA WASAKWA

WANAOTAPELI KWA JINA LA MAMA SALMA WASAKWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Imeandikwa na Mwandishi Wetu
JESHI la Polisi nchini limewataka Watanzania kutoa ushirikiano kuwapata wahusika wa kikundi cha vikoba kiitwacho Focus Vicoba Tanzania kwa kuwa ni cha kitapeli.
Msemaji wa Jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa, alisema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana kuwa, kikundi hicho kinatumia majina ya viongozi ikiwemo Mama Salma Kikwete, kufanya utapeli.
“Katika siku za karibuni kumejitokeza vitendo vya baadhi ya watu kutumia majina ya viongozi ama wake wa viongozi wa nchi kufanya utapeli unaohusisha wizi wa fedha kwa njia ya mtandao,” alisema Mwakalukwa.
Alisema uchunguzi wa jeshi hilo umebaini uwepo wa kikundi cha Focus Vicoba Tanzania ambacho kinatangaza kuwa kipo chini ya uongozi wa Mama Salma Kikwete (mke wa Rais Mtaafu, Jakaya Kikwete, sasa Mbunge), kuwatapeli watu kuwa kinatoa mikopo kwa wanachama wanaojiunga nacho.
Alisema Polisi inatoa mwito kwa wote waliotapeliwa na kikundi hicho kutoa taarifa kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), au Kamanda wa Polisi Mkoa, ama katika Kituo cha Polisi chochote cha karibu ili kutoa ushirikiano kwa ajili ya taratibu za kiuchunguzi kuwabaini wahusika.Awali kikundi hicho kiliwahi kuripotiwa kikijitangaza kuwa kinamilikiwa na Mkurugenzi wa Kampuni za IPP kwa utapeli kama huo.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa