Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe
akizungumza na wasanii wa nyimbo za Bongo Freva hapa nchini kuhusu
maswala mbalimbali yanayowahusu wasanii hao, pia wameshauliwa kujiunga
kusajili kazi zao pamoja na kulipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA), kupata miongozo mbali mbali COSOTA pamoja na BASATA.
Baadhi
ya wasanii wa Nyimbo za Bongo Freva hapanchini kutoka kulia ni Wastara
Thomasi, msanii wa Bongo Fleva, Khadija Shaban (Keisha) na Witnes
Mwajaga wakiwa katika Mkutano wa wasanii wa Bongo freva na Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe jijini Dar
es Salaam leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe
akipokea saa ya ukutani ikiwa ni Rambirambi kutoka kwa wasanii wa Mziki
wa Bongo Freva kama pole kufiwa na Mkewe.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
Wasanii wa Bongo Freva hapa nchini wameaswa kukuzingatia matumizi ya Lunga pamoja na mavazi ili kuepushafungia fungia ya kazi zao za sanaa hayo yamesemwa leo wakati wa mkutano wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na wasanii wa nyimbo za bongo Freva pamoja na wadau mbalimbali na sanaa hapa nchini jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment