Imeandikwa na Halima Mlacha
KATIKA jitihada za kuwadhibiti wafanyabiashara wa mashamba makubwa
wanaoyatumia kwa ajili ya kukopea fedha na kisha kutoyaendeleza,
serikali inatarajia kuanzia mwakani, kuwasilisha bungeni Muswada wa
Marekebisho ya Sheria ya Ardhi, utakaowadhibiti wafanyabiashara hao.
Hatua hiyo, imetokana na namna Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo
ya Makazi, ilivyobaini uwepo wa mashamba mengi yakiwemo yanayomilikiwa
na wafanyabiashara wakubwa nchini ambayo hayajaendelezwa huku yakiwa
yamekopewa fedha nyingi na kutumika katika biashara nyingine.
Akizungumza na magazeti ya Serikali ya HabariLeo na Daily News
ofisini kwake Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Moses Kusiluka alisema sheria hiyo
italenga kudhibiti watu kutumia mashamba kujipatia fedha na kisha
kuyatelekeza.
“Tunataka kupitia sheria hii, mtu akikopa kupitia mashamba haya,
fedha hizo zitumike kuyaendeleza na siyo kuyaacha mapori na kufanya
biashara zake nyingine. Sheria itaweka masharti kuwa mikopo yote yenye
dhamana ya mashamba, isimamiwe na benki zenyewe,” alisema.
Alisema katika mpango unaoendelea wa kushirikiana na halmashauri za
wilaya kufanya ukaguzi wa mashamba yasiyoen-delezwa wamebaini mashamba
mengi ambayo hayajaendelezwa yakiwemo yaliyochukulia mikopo benki.
“Mashamba yote yasiyoendelezwa baada ya kufuata taratibu zote, ikiwemo
kutoa notisi kwa wamiliki tumeyawasilisha kwa Rais John Magufuli kwa
ajili ya kubadilishiwa umiliki.
Haya yaliyochukulia mikopo, sheria inaturuhusu kuyataifisha pia,”
alisema. Hata hivyo, alisema mashamba hayo yaliyochukulia mikopo kwa
sasa wanazungumza na benki husika ili kuangalia namna ya wahusika wa
mashamba hayo kubadili dhamana za mikopo yao ili yaweze kurejeshwa
mikononi mwa serikali.
“Tunafanya hivi si kwa sababu eti hatuna uwezo wa kuyachukua la
hasha, tunafanya hivi ili kunusuru benki hizi, kwani mashamba mengi
yamechukulia mikopo mikubwa endapo tutayataifisha na kuyachukua kama
hakuna dhamana nyingin
CHANZO HABARI LEO
0 comments:
Post a Comment