Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dk Hamis Kigwangala amezitaka Sekretarieti za mikoa na halmashauri zote nchini kuhakikisha kwamba inawashirikisha wananchi katika maandalizi ya bajeti kubuni vyanzo vya mapatao.
Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bungeni leo kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha 2013, mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Kigwangala amesema pia wananchi washirikishwe katika utungaji wa sheria ndogo za ukusanyaji ili kurahisisha zoezi la makusanyo bila manung’uniko.
Amesema ushiriki wa wananchi pia utasaidia katika zoezi zima la kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo hasa pale ambapo Serikali kuu pamoja na Serikali za Mitaa zitakapokuwa zinatoa mchango wake kikamilifu katika miradi husika na hivyo nguvu ya wananchi kutopotea.
No comments:
Post a Comment