Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm amebwaga manyanga kuendelea
kuinoa timu hiyo baada ya kupata ‘ofa’ ya kuinoa klabu ya Al Shoala
Sports ya Saudi Arabia.
Akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya
klabu ya Yanga jana, Pluijm alisema ofa hiyo ni kubwa na roho inamuuma
kuicha Yanga ambayo tayari ni mwanachama, lakini hana jinsi.
“Ofa ni kubwa sana, yeyote asingevumilia na nimezungumza na viongozi wa Yanga, wamekubaliana na hilo.
“Naondoka kwenda Ghana mchana huu kuwasaidia Yanga
kusaka wachezaji ambao watawasaidia msimu ujao. Nitahakikisha
nawatafutia wachezaji wazuri kuliko hawa walionao.”
Pluijm ameinoa Yanga kwa miezi sita na kuiwezesha
kushika nafasi ya pili, na alisema tayari ameshasaini mkataba wa mwaka
mmoja na Al Shoala Sports.
Akifafanua kuondoka kwake iwapo ametofauatina na
viongozi, Pluijm alisema: “Nina masikitiko moyoni kuiacha nchi nzuri ya
Tanzania. Ninawashukuru wote, wachezaji, wanachama, viongozi wa Yanga na
Watanzania wote kwa ujumla. “Kabla sijaja kuifundisha Yanga, meneja
wangu alipata ofa kubwa Saudi Arabia na nikasaini mkataba wa mwaka
mmoja, lakini uongozi wa timu ninayoenda kuifundisha (Al Shoala),
walikuwa na matatizo na kocha aliyekuwapo, hivyo wakaniomba nisubiri
mkataba wake uishe ndiyo na mimi nijiunge nao.
“Mkataba wake umeisha na mimi naanza kazi rasmi
Julai. Mkataba wangu utamalizika baada ya mwaka mmoja. Itategemea kama
Yanga watakuwa bado wananihitaji, na kama ofa yao itakuwa nzuri,
nitarudi.”
Naye katibu mkuu wa Yanga, Benno Njovu alisema
wamebariki kundoka kwa Pluijm kwa vile tayari alishapata kazi Saudi
Arabia na ameshasaini mkataba, hivyo wapo kwenye harakati za kusaka
kocha mwingine wa kuziba pengo la kocha huyo, ambaye alianza kazi
Januari akichukua mikoba ya Ernie Brandts.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
No comments:
Post a Comment