Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Slaa
Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Angelina Malembeka, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi na Huduma za Jamii manispaa hiyo.
Alitoa kauli hiyo wakati akizungumza kwa niaba ya Meya wa Ilala, Jerry Slaa, (pichani) kwenye mkutano mkuu wa wa Y2K Social Klabu iliyoanzishwa kwa lengo la kushughulikia kero zinazo ikabili jamii ya kata ya Kiwalani.
Angelina alisema kumekuwapo na malalamiko mengi yanayofika manispaa, lakini wanapotoa onyo kwa wamiliki wa viwanda yamekuwa hayatekelezwi na wahusika.
Angelina alisema baadhi ya viwanda pamoja na uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kuwa ni moja ya maeneo yanayotiririsha maji machafu kwa wananchi kwa kipindi kirefu sasa.
“Sasa kitakachofuata ni kufungia viwanda na maeneo yote sugu yanayochafuwa mazingira kwa makusudi na kuhatarisha maisha ya wananchi,” alisema Angelina.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Mwenyekiti wa Y2K Social Klabu, Fatma Mwasora, alisema toka kuanzishwa kwa klabu hiyo wamekuwa wakipambana na changamoto za kuweka mazingira ya Wilaya ya Ilala katika hali ya usafi na kwamba kwa kiwango kikubwa lengo hilo limefanikiwa.
“Changamoto ni nyingi hasa kwenye vituo vya afya kumekuwa na rushwa ambazo zinawakatisha tamaa wananchi kuamini huduma zinazotolewa na watendaji wa Serikali,” alisema Fatma.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment