Thursday, July 10, 2014

MSICHANA AKUTWA KALALA KWENYE SANDUKU LA MCHOMA CHIPS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Kituko hiki kilitokea huko pande za Yombo Vituka Dar-Es-Salaama mchoma chips kama kawaida baada ya kumaliza biashara yake alifunga kabati lake kwa kufuli na kwenda kulala.
 Cha kushangaza alivyo amka asubuhi na kuja kufungua kabati lake, alikuta huyu dada kalala ndani ya kabati akiwa hajitambui na bila hata kula mabaki ya chips na mishkaki kama unavyoona. kitu kilicho waacha majirani midomo wazi wasijue la kufanya. Na hadi sasa bado haijajulikana aliingiaje ndani ya kabati hilo la muuza chips kwani aliondoka bila hata kusema chochote.

No comments:

Post a Comment