Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi wa kampuni ya Frontline Porter
Novelli ambaye nia ni mtetezi wa haki za wanawake nchini Bi Irine Kiwia
amesema katika kuhakikisha wanawake wanapiga hatua za kimaendeleo nchini
ni jukumu la wadau wa maendeleo nchini kuweka mikakati endelevu kwa
kushirikiana na serikali ili kuhakikisha usawa wa wanawake unapatikana.
Bi Kiwia ameyasema hayo alipokuwa akizungumza kuhusu siku ya wanawake dunuiani na nafasi ya wanawake katika jamii yetu.
''Wapo wanawake ambao ni wasomi na
wanauwezo wa kushika nyazifa mbalimbali katika jamii ni vyema wapewe
nafasi hizo siyo kwa kigezo cha mwanamke bali kutokana na uwezo wao na
ujuzi katika ngazi husika''-Amesema Bi Kiwia
Vilevile Kiwia ameitaka serikali kutizama
sheria ambazo bado hazitoi fursa jkwa wanawake katika kujikwamua
kiuchumi na kiutamaduni mfano sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo ambayo
inatoa ruhusa kwa mwanamke kuolewa akiwa na umri chini ya miaka 18.
Aidha amewataka wanaharakati na serikali
kwa ujumla kuunganisha nguvu zao pamoja ili kuhakikisha haki ya mwanamke
inapatikana kwa kupinga mila potofu za kumkandamiza mwanamke ambazo
zimeota mizizi katika jamii.
No comments:
Post a Comment