Ugonjwa wa Kipindupindu umeendelea kusambaa nchini licha ya serikali kwa kushirikiana na mashirika mbalimbali kuonyesha nia ya kupambana na ugonjwa huo ambao mpaka sasa umesababisha zaidi ya watu 290 wamepoteza maisha.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Huduma za Kinga wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Neema Rusibamayila alisema serikali imekuwa ikiendelea kutoa fedha ili kupambana na ugonjwa huo ambao unaonekana kuzidi kuwa tishio kwa maisha ya watanzania.
Alisema serikali imeshatoa milioni 900 kwa ajili ya kusaidia mapambano ya Kipindupindu ambapo fedha hizo zimekuwa zikitumika kununua dawa, kusaidia vituo vya afya ambavyo vinawahudumia wagonjwa wa Kipindupindu na kuziwezesha timu za uelimishaji kuhusu kipindupindu kufikia maeneo mengi zadi.
“Serikali imekuwa ikiunga mkono mapambano na kuhusu gharama Wizara ya Afya ilishapokea Milioni 900 kutoka hazina kwa ajili ya kusaidia kupambana na Kipindupindu,” alisema Dkt. Rusibamaliya.
DSC_1453Mkurugenzi wa Huduma za Kinga wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Neema Rusibamayila  akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema pamoja na fedha hizo lakini pia kuna mashirikia yamekuwa yakiwasaidia ambayo ni pamoja na UNICEF ambao wameshatumia  Bilioni mbili ambazo zilitumika kununua vifaa zikiwepo dawa za kuulia vijidudu kwenye maji, vitanda na vituo vya kutolea dawa.
Mashirika mengine ni CBC wao walitoa wataalamu wa afya, Red Cross walitoa vifaa, vitanda, wataalamu wa afya na watu waliojitolea kusaidia uelimishaji na CMF ambao nao walitoa vifaa tiba na dawa kwa wagonjwa.
Nae Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Michael John alisema katika kipindi cha wiki moja iliyopita walipokea taarifa za kuwepo kwa wagonjwa wapya 758 ambao ni asilimia 40 zaidi ya taarifa ya wiki mbili zilizopita ambapo walipokea taarifa za wagonjwa 544.
DSC_1438Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Michael John akielezea jambo katika mkutano na waandishi wa habari.
Aidha John aliwataka viongozi wa dini kutumia nafasi yao katika jamii kwa kuwaelimisha waumini wao kuhusu ugonjwa wa Kipindupindu na waache imani potofu kutokana na baadhi ya maeneo kuacha kuchemsha maji kutokana na kuwa na imani ambazo siyo za kweli.
DSC_1433Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Michael John akitoa taarifa ya kipindupindu kwa muda wa wiki moja iliyopita katika mkutano na waandishi wa habari.
DSC_1435
DSC_1429