Home » » JK AKABIDHI JWTZ VITABU 2,181

JK AKABIDHI JWTZ VITABU 2,181

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

RAIS Jakaya Kikwete, amekabidhi vitabu 2,181 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya vyuo vya Jeshi ili kuongeza taaluma.
Rais Kikwete, alikabidhi vitabu hivyo kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange, Ikulu Dar es Salaam jana na ameahidi kuendelea kutafuta vitabu zaidi kwa ajili ya kuboresha Maktaba ya Jeshi iliyopo katika Chuo cha Kijeshi kilichopo Monduli mkoani Arusha.
Maktaba hiyo ilianzishwa na Rais Kikwete, wakati alipokuwa mkufunzi katika chuo hicho miaka iliyopita.
“Lazima mtenge bajeti kwa ajili ya vitabu, lakini na mimi nitaendelea kutafuta vitabu niwaletee ili kuijengea uwezo Library (maktaba) yetu ya Monduli,” alisema Rais Kikwete.
Akipokea vitabu hivyo kwa niaba ya Jeshi, Jenerali Mwamunyange, alimshukuru Rais kwa juhudi zake za kuboresha Jeshi la Wananchi Tanzania kwa ujumla na kulifanya kuwa la kisasa zaidi. “Juhudi zako za kuliendeleza Jeshi letu imetuongezea uwezo na kujiamini zaidi. Bila juhudi zako tusingefika hapa tulipo na tunajivunia sana mafanikio haya,” alisema Jenerali Mwamunyange

 Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa