Home » » TANESCO YAKAMILISHA MIRADI 10 YA JICA

TANESCO YAKAMILISHA MIRADI 10 YA JICA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco), limekamilisha miradi kadhaa ya umeme kwenye maeneo mbalimbali nchini kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Japan (Jica).
Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco, Adrian Severin alisema mwishoni mwa wiki kwamba miradi mikubwa zaidi ya 10 iliyofadhiliwa na JICA imeshakamilika tangu mwaka 1984 hadi sasa.
Aliitaja miradi ambayo imekamilika kuwa ni ule wa mfumo wa usafirishaji umeme na usambazaji katika Mkoa wa Kilimanjaro uliogharimu Sh28 bilioni.
Alisema Tanesco ilikamilisha mradi wa kuimarisha mfumo wa usambazaji umeme kwa jiji la Dar es Salaam mwaka 1991kwa msaada wa JICA Sh63.4 bilioni.
Severin aliitaja miradi mingine na gharama na mwaka wa kukamilika kwake kuwa ni pamoja na wa umeme Mkoa wa Kilimanjaro (1997 – Sh 7.8 bilioni), Mradi wa kupanua upatikanaji wa umeme kwa Mkoa wa Dar es Salaam kwenye vituo vya kupooza umeme vya Ilala, Mbagala, ujenzi wa Kituo cha Kariakoo na njia ya msongo wa kilovolti 132 Ubungo hadi Ilala awamu ya kwanza (1998 – Sh 18.5 bilioni).
Mradi mwingine maarufu ni ujenzi wa kilometa saba za msongo wa kilovolti 132 kutoka Ubungo hadi Makumbusho (2011 – Sh 7.3 bilioni), ukarabati wa kituo cha msongo wa kilovolti 132/33 cha Ilala (2013 – Sh827 milioni), ukarabati mkubwa wa kituo cha kupooza umeme na njia za usafirishaji umeme Mkoa wa Kilimanjaro (2013 – Sh40.6 bilioni).
Severin alitaja miradi mingine ambayo inaendelea kuwa ni ujenzi wa mradi mkubwa wa uwekezaji kwenye usafirishaji umeme kutoka Iringa - Dodoma – Singida – hadi Shinyanga wa kilometa 217, kilovolti 400 maarufu kama backbone ulionza mwaka jana kwa gharama ya Dola za Marekani 26 milioni unaotarajiwa kukamilika mwaka 2016.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa