Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dk. Titus Kamani
Dk. Kamani aliyasema hayo wakati akifungua mkutano wa wadau wa tasnia ya ngozi uliofanyika jana jijini Dar es Salam.
Alisema licha ya Tanzania kuwa nchi ya pili uwingi wa mifugo barani Afrika baada ya Ethiopia kwa kuwa na ng`ombe milioni 22.8, mbuzi 15.6 na kondoo 7.0, lakini kipato kinachopatikana kutokana na bidhaa ya ngozi ya mifugo hiyo hailingani na idadi ya mifugo iliyopo.
Alisema kwa utafiti wa mwaka 2013 uzalishaji wa vipande vya ngozi ya Ng`ombe umeshuka kutoka milioni 3.4 hadi 2.9, Mbuzi 4.4 hadi 3.6 na Kondoo milioni 2.0 hadi 700,000.
Alitaja sababu kubwa zinazochangia sababu kubwa inayochangia uzalishaji wa ngozi ni kutokana na kutokuwa na viwanda vya kutosha vya usindikaji wa ngozi pamoja na utoroshaji wa ngozi kwenda katika jirani kupitia njia za panya.
Aidha, alisema kuwa serikali inajipanga kuhakikisha shughuli za uzalishaji na usindikaji wa bidhaa hiyo zinafanyika hapa hapa nchini kuanzia hatua ya awali mpaka ya mwisho, ili kuhakikisha taifa linanufaika kiuchumi tofauti na ilivyyo sasa.
Alisema mpaka sasa uzalishaji unaofanyika nchini unaishia katika hatua ya awali tu ya wet bluu, ambayo haina faida yeyote.
CHANZO:
NIPASHE
No comments:
Post a Comment