Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wabunge wa Bunge la Bajeti linaloanza kesho mjini Dodoma, wamepunguziwa muda zaidi wa kuchangia kutoka dakika 15 hadi saba.
Bunge hilo la Bajeti limetengewa siku chache ambazo zitalilazimu kuendeshwa kwa kasi ili kukamilisha shughuli zake.
Habari zilizopatikana jana zilisema hatua hiyo
inatokana na muda kuwa mfupi kwa kuwa Bunge hilo litakutana kwa siku 52
ikiwa ni pungufu ya siku 28 ikilinganishwa na mkutano kama huo wa mwaka
jana.
Katibu wa Bunge, Thomas Kashililah alipoulizwa
kuhusu taarifa hiyo jana alisema ofisa habari wa Bunge, Owen Mwandumbya
angeweza kulizungumzia. Hata hivyo, Mwandumbya alipoulizwa alisema
atazungumza leo.
Miongoni mwa marekebisho yaliyopitishwa katika
kupunguza muda wa vikao ni pamoja na kuendelea kufanyika hadi Jumamosi
pia kumalizika saa 2:00 usiku.
Ratiba iliyotolewa na Bunge imesema utaratibu wa
sasa unalilazimisha lifanye uamuzi wake (kupitisha au kutokupitisha),
Bajeti ya Serikali pamoja na Sheria za Fedha ifikapo mwishoni mwa Juni
kila mwaka, ili kuruhusu utekelezaji wa bajeti husika kuanza Julai Mosi,
siku ya kwanza ya mwaka mpya wa fedha.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
No comments:
Post a Comment