Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete ametuma salama za rambirambi kwa mama Maria Nyerere na
familia yake kwa kuondokewa na mmoja wa wana familia yake, Bw. John
Nyerere aliyefariki Jumamosi Mei 9,2015 katika Hospitali ya Muhimbili
jijini Dar es Salaam
Pamoja na
salamu hizi, Rais Kikwete ambaye yuko nchini Alrgeria kwa ziara ya
kikazi, amefanya mawasiliano binafsi na Mama Maria na kumpa pole kwa
kuondokewa na kijana wake.
“Hakuna
mzazi anayependa kuondokewa na mwanae, ni kitu kigumu sana kwa mzazi
kukishuhudia , hivyo naelewa maumivu na huzuni kubwa uliyo nayo”. Rais amemwambia Mama Maria na kumuomba akaze moyo na kumuombea Marehemu John apate pumziko la milele.
Rais
Kikwete amemhakikishia Mama Maria kuwa yeye binafsi pamoja na familia
yake , wapo nae katika kipindi hiki kigumu na kuwa watashirikiana wote
katika msiba huu kwa hali na mali.
Rais Kikwete anatarajia kuwasili nchini leo usiku.
Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu – Dar es Salaam.
11 Mei, 2015
0 comments:
Post a Comment