Home » » Rais Kikwete aomboleza kifo cha John Nyerere

Rais Kikwete aomboleza kifo cha John Nyerere

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
jon
Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salama za rambirambi kwa mama Maria Nyerere na familia yake kwa kuondokewa na mmoja wa wana familia yake, Bw. John Nyerere aliyefariki Jumamosi Mei 9,2015 katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam
Pamoja na salamu hizi, Rais Kikwete ambaye yuko nchini Alrgeria kwa ziara ya kikazi, amefanya mawasiliano binafsi na Mama Maria na kumpa pole kwa kuondokewa na kijana wake.
“Hakuna mzazi anayependa kuondokewa na mwanae, ni kitu kigumu sana  kwa mzazi kukishuhudia , hivyo  naelewa maumivu na huzuni kubwa uliyo nayo”. Rais amemwambia Mama Maria na kumuomba akaze moyo na kumuombea Marehemu John apate pumziko la milele.
Rais Kikwete amemhakikishia Mama Maria kuwa yeye binafsi pamoja na familia yake , wapo nae katika kipindi hiki kigumu na kuwa watashirikiana wote katika msiba huu kwa hali na mali.
Rais Kikwete anatarajia kuwasili nchini leo usiku.
Imetolewa na;
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi,
Ikulu – Dar es Salaam.
11 Mei, 2015

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa