Home » » NITAJIPIMA KAMA NAFAA MWAKA 2020- HALIMA MDEEE

NITAJIPIMA KAMA NAFAA MWAKA 2020- HALIMA MDEEE

Mh. Halima Mdee Mbunge wa Jimbo la Kawe, Picha na Fredy 
Njeje/Blogs za Mikoa

Na Godfriend Mbuya
Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia CHADEMA Halima James Mdee amesema kama Mungu akimpa uhai mwaka 2020 katika uchaguzi Mkuu atajipima kama ametekeleza ahadi za wananchi kama alivyoahidi ndipo atagombea kama atakuwa hajafikisha asilimia 50 ataachia mtu mwingine.

Akizungumza katika kipindi cha HOTMIX kinachorushwa na EATV Mdee amesema, Mwaka 2020 hatakuwa na sababu ya msingi ya kugombea kama hajaweza kufanya kitu kwa wananchi wa jimbo lake.

“Nitaangalia kama nimefikia asilimia 50% ya utekelezaji wa ahadi za wananchi ndipo nitafanya hivyo ila nisipotekeleza nitapisha ili mtu mwingine mwenye maono zaidi ya ya kwangu aweze kugombea na kuongoza jimbo hilo”-Amesema Mdee

Aidha Mdee amesema  kwa sasa nimefanikiwa kutatua baadhi ya kero za wananchi kama maji katika baadhi ya maeneo, na barabara nyingine zimetengewa fedha na serikali hivyo zitajengwa na kwenye ardhi amefanikiwa kwa kushirikiana na wananchi kutatua  migogoro ya adrhi katika maeneo ya Magwepande, Bunju, na Kunduchi  ambapo bado naendelea na kazi hiyo katika maeneo mengine.

Kwa upande mwingine Mdee amesema suala la kufanya mikutano ya hadhara atafanya kulingana na Katiba na sheria za nchi zinavyoruhusu na si vinginevyo.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa