Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » NEWS ALERT: MAHAKAMA KUU YAMUACHIA HURU SHEIKH PONDA LEO

NEWS ALERT: MAHAKAMA KUU YAMUACHIA HURU SHEIKH PONDA LEO


Sheikh Ponda akiwa ndani ya Mahakama Kuu akisubiri hukumu.
Wakili wa Sheikh Ponda, Bw Juma Nassoro akizungumza jambo na mteja wake mahakamani hapo.
…. Nassoro akiteta jambo na Sheikh Ponda.
Askari akidumisha ulinzi mahakamani hapo.
Sheikh Ponda  akitoka nje ya Mahakama Kuu baada ya kushinda Kesi ya Ardhi iliyokuwa ikimkabili kisha kurudi mahabusu katika gereza la Segerea.
….akipanda Karandinga  la magereza.
Sheikh Ponda akiwa ndani ya gari la magereza tayari kwa kurudi rumande.
MAHAKAMA  Kuu ya Tanzania imemuachia huru aliyekuwa Katibu wa Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda baada ya kuona hana hatia dhidi ya Kesi ya madai ya Ardhi ya Agrekanza inayomilikiwa na Afidhi Self  iliyokuwa inamkabili.
Akisoma Mashtaka hayo Mwanasheria wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Jaji, Augustino Shangwe alisema baada ya kupitia vifungu vyote mahakama imejiridhisha na kuona Sheikh Ponda hana hatia yoyote na kumuachia huru tangu leo lakini katika hali ya kushangaza Sheikh Ponda amerudishwa rumande akisubiri kesi nyingine ya madai ya uchochezi,  Mkoani Morogoro inayomkabili.
Kujua mengi yaliyojiri mahakamani hapo tembelea www.globatvtz.com
(PICHA/HABARI : DEOGRATIUS MONGELA/GPL)
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa