SERIKALI KUFUNGUA FURSA ZA AJIRA KUPITIA MIKATABA MITANO




Na Mwandishi - KAM Dar es salaam
 
Mikataba 16 ya Ajira Kimataifa ipo Katika Hatua za Mwisho

Serikali Kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano imesaini Mikataba Mitano ambayo itawawezesha wananchi kupata ajira Nje ya Nchi.

Hayo yamesemwa Februari 7, 2026 Jijini Dar es salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu wakati wa Hafla ya Chakula cha Jioni (Gala Dinner) kilichohusisha uzinduzi rasmi wa kipindi cha  Imbeju- Bongo Fursa na Jarida la Mapitio ya Vijana  lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Biashara na Maendeleo.

“Nlikuwa Falme za Kiarabu nimekutana na Mawaziri wa Kazi kutoka Nchi Mbalimbali na wote walionyesha nia nzuri na nchi yetu, hadi sasa tumesaini Mikataba mitano ambayo iko tayari yamashirikiano na nchi hizi kwa ajili ya Fursa za Ajira kwa Vijana” amesema.

Aidha Mhe. Sangu amesema fursa zilizotajwa kwenye Dira ya Taifa zinapatikana kupitia Wizara hiyo na Serikali inafanya mazungumzo ya mwisho kwenye Mikataba 16 ya Ajira kwa ajili ya Watanzania.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa NEDC, Jesse Madauda Amesema lengo la Jarida na Kipindi chicho  ni kuwatia Moyo vijana na Kuwafikia wawekezaji ili waone vijana wa Kitanzania wanafanya shughuli za kibunifu na hatua walizofikia ili iwe rahisi kuwafikia wajasiriamali hao.

Awali akizungumza Mmoja wa Wajasiriamali Elizabeth Consoli ameishukuru serikali kwa kuwa pamoja na wajasiriamali wavumbuzi  na kuonyesha nia ya kuwavusha wajasiriamali hao kutoka hatua Moja kwenda Hatua nyengine.


TAARIFA KWA UMMA - ZOEZI LA UHAKIKI WA WASTAAFU NA WATEGEMEZI



 

Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni awasili Ikulu Jijini Dar es Salaam

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 07 Februari, 2026. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2026. 

Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akisaini Kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 07 Februari, 2026. 

FURSA AJIRA QATAR ZAVUTIA VIJANA WENGI



Na. OWM - KAM (DSM)

Mamia ya Vijana kutoka Mikoa mbalimbali nchini wamejitokeza katika Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kushiriki zoezi la usajili wa madereva wanaotarajia kwenda kufanya kazi nchini Qatar.

Zoezi hili ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya Serikali ya kuwaunganisha Watanzania na fursa za Ajira nje ya nchi kupitia mifumo rasmi ili kuhakikisha ulinzi wa haki na usalama wao.

Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ajira, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Jane Sorogo, amebainisha kuwa mwitikio umekuwa mkubwa ambapo zaidi ya Vijana 1,700 wamejitokeza kuomba nafasi hizo licha ya mahitaji kuwa ni madereva 1,500 pekee.

Akizungumza wakati wa ziara yake chuoni hapo tarehe 06 Februari 2026, Waziri wa Nchi hiyo Mhe. Clement Sangu, amesema Serikali imeweka mifumo imara ya kisheria inayosimamia Ajira hizo ili kulinda maslahi ya Watanzania.

Waziri Sangu pia amebainisha kuwa tangu mwezi Novemba 2025 hadi Januari 2026, jumla ya Watanzania 2,019 wameunganishwa na fursa za Ajira katika nchi za Saudi Arabia, Qatar, Oman, Falme za Kiarabu na kwingineko.

Aidha, amesema Serikali iko mbioni kusaini hati za makubaliano na nchi nyingine 16 ili kuzidi kutanua wigo wa Ajira kwa vijana.

Mhe. Sangu ametoa wito kwa vijana kuendelea kuchangamkia fursa hizo kupitia njia rasmi za Serikali na kuepuka mawakala wasio rasmi kwa maslahi ya usalama wao na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza kwa niaba ya waombaji, mmoja wa madereva waliojitokeza, Hassan Mohamed, amesema ameamua kufuata utaratibu huo rasmi kwa kuwa unatoa uhakika wa ulinzi wa haki na maslahi yake akiwa ugenini.

Juhudi hizi zinaonyesha dhamira ya Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu katika kutengeneza mifumo inayotoa matumaini na usalama kwa nguvu kazi ya kitanzania inayotafuta fursa nje ya mipaka.

IAEA yajionea mageuzi ya utoaji huduma katika Taasisi ya Ocean Road


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kiufundi kwa Afrika Gashaw Gebeyehu Wolde wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA)akizungumza na waandishi  wa habari mara baada ya kutembembelea mashine za kisasa katika Taasisi ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Mtendaji  Mkuu wa Taasisi ya Ocean Road Dkt.Diwani Msemo akizungumza kuhusiana na mikakati ya Taasisi mara baada ya kutembelewa na IAEA jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Profesa Najat Kassim Mohammed akizungumza kuhusiana na ujio wa IAEA katika Taasisi ya Ocean Road kuangalia mashine za miozi, jijini Dar es Salaam.


*Waahidi kuwa wa kwanza kudhibitisha Ithibati ya ubora.

Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA) limesema kuwa Taasisi ya Ocean Road imefanya mageuzi katika utoaji huduma za saratani.

Akizungumza katika ziara ya Shirika hilo likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kiufundi kwa Afrika Gashaw Gebeyehu Wolde amesema Taasisi ya Ocean Road katika imefanya mageuzi makubwa ya kuwa na vifaa vya teknolojia katika otoaji wa huduma za Saratani ikilinganishwa na miaka iliyopita wakati walipotembelea.

Wolde amesema katika hatua ambayo imefikiwa watakuwa watu kwanza katika kupitisha ithibati ya ubora ya huduma ya Saratani na kufanya Taasisi ya Ocean Road kuwa ya Tatu Afrika katika utoaji huduma hiyo.

Amesema Serikali ya Tanzania imewekeza katika kuwa na miundombinu pamoja na vifaa vya Kisasa ikiwemo za ugunduzi wa saratani za aina mbalimbali.

Aidha amesema IAEA itaendelea kutoa ushirikiano kwa Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) ili kuimarisha ushirikiano, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya matumizi ya mashine za CT-Scan na kutoa vifaa vya mionzi na kusomesha wataalam katika ubobezi wa magonjwa ya saratani.

Hata hivyo Wolde ametoa shukurani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa ununuaji wa mashine za kisasa na fedha nyingi katika Taasisi ya Ocean Road.

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Ocean Road Dkt.Diwani Msemo amesema kuwa ujumbe IAEA wametembelea mashine mbalimbali na kuona Taasisi hiyo imejipanga.

Amesema miundombinu na vifaa tiba vilivyopo vimeongeza huduma katika kutoa huduma kwa mgonjwa bila kuathiri .

Hata hivyo amesema ujumbe huo umekiri kuwa mashine zilizopo za kisasa katika hospitali za Afrika Mashariki.

Mkurugenzi Mkuu wa Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Profesa Najat Kassim Mohammed amesema Taasisi ya Ocean Road imepiga hatua kubwa katika utoaji wa huduma ya Saratani.

Aidha ametoa shukurani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika uwezeshaji wa vifaa vya kisasa katika Taasisi ya Ocean kwa kutumia Fedha za ndani.

UTEUZI


 



Serikali Yasajili Anwani za Makazi Milioni 12.9

Na Timothy Mwakyenda-   MAELEZO

Serikali imesajili zaidi ya Anwani za Makazi Milioni 12.9 ili kuyatambua maeneo mbalimbali na kuyarasimisha kwenye mfumo wa kidijitali.

Takwimu hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Nicholas Merinyo Mkapa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Bw. Mohamed Hamis Abdullah leo Februari 6, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo jijini Dar es salaam ikiwa ni mwendelezo wa Kongamano la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta.


"Tanzania ilianza mchakato wa usajili wa Anwani za Makazi nchi nzima tangu mwaka 2010, hadi  kufikia mwaka 2026 imefanikiwa kusajili zaidi ya anwani milioni 12.9", amesema Naibu Katibu Mkuu, Mkapa.

Naibu Katibu Mkuu Mkapa ameongeza kuwa, Anwani za Makazi ni kitovu cha maendeleo kwa nchi kwa sababu zinatambua na kuunganisha maeneo mbalimbali ya nchi na kuziweka pamoja katika mfumo wa kidijitali ambapo toka zoezi la usajili lianze, jumla ya mifumo 29 imeunganishwa ikiwemo Shirika la Posta.


Ametoa rai kwa washiriki wa kongamano hilo kuwa katika siku za majadiliano, wajumbe waweke mkazo katika kujadili namna ambavyo Anwani za Makazi zina umuhimu katika utoaji wa huduma za afya, elimu na kukuza uchumi.

Aidha, Mkapa amesisitiza kuwa mifumo imara ya Anwani za Makazi huimarisha utu wa watu na kuibua fursa za kimaendeleo kwa watu wote. 


MHE. DKT SAMIA AREJEA TANZANIA

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akitokea Dubai, tarehe 6 Februari, 2026. alipokuwa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).

Mhe. Rais Dkt. Samia alishiriki katika Mkutano wa Dunia wa Serikali (World Governments Summit – WGS) 2026 pamoja na Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa wa Uwekezaji Afrika (GAIS).
___
#TanzaniaNaUwekezaji
#DiplomasiaYaKiuchumi
#KaziNaUtuTunasongaMbele

RAIS WA JAMHURI YA UGANDA KUTUA TANZANIA


 

RAIS DKT SAMIA KUZINDUA SOKO LA KARIAKOO FEBRUARI 08, 2026

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajia kuzindua soko la Kariakoo  Februari 8, 2026 ambalo lilikuwa kwenye ukarabati baada ya kuungua na moto na Soko jipya ambalo limejengwa

Akizungumzia ujio wa  Rais Dkt Samia RC Chalamila amesema soko hilo kwa sasa limekamilika kwa asilimia 100 ambapo zaidi ya shilingi bilioni 28 zimetumika kukarabati na kujenga soko jipya likiwa na takribani vizimba zaidi ya 1500 kwa ajili ya wafanyabiashara

RC Chalamila amewataka wananchi wakazi wa Mkoa huo, wafanyabiashara wadogo wa kati na wakubwa kujitokeza kwenye uzinduzi huo wa Soko la kariakoo ili kumuunga mkono Rais Dokta Samia lakini pia kuweka historia ya tukio hilo kubwa linalotarajiwa kuwa ni kiungo muhimu katika kujenga uchumi wa Mkoa huo na Taifa kwa ujumla

Aidha Chalamila ameagiza wafanyabiashara wadogo ambao wamefunga barabara za kuingia soko la kariakoo waondoke na waache barabara hizo wazi kabla ya februari 8 ili kuruhusu wafanyabiashara  kuingia kwenye Soko hilo.


 

Wanawake wametakiwa kuzingatia uvaaji wa viatu vyenye kisigino kifupi

 Wanawake wametakiwa kuzingatia uvaaji wa viatu vyenye kisigino kifupi kuimarisha afya ya miguu na kuepuka kuvaa viatu vyenye kisigino kirefu ama kisigino flati ambavyo ni hatari kwa afya ya magoti. 


 Akizungumza na wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) kanda ya Mabibo katika kambi ya matibabu ya siku mbili ya uchunguzi wa afya Mtaalamu wa mazoezi tiba kutoka JKCI Jaqline Mariki alisema mtu anatakiwa kuvaa viatu vyenye kisigino kifupi ili unyayo uweze kunyanyuka kidogo kusaidia ugawanyishwaji wa uzito kwenye mwili hivyo kutoleta maumivu katika mwili.


 

MALKIA NA BALKIA WACHANGAMKIA FURSA YA KUJIWEKEA AKIBA NA NSSF

Katika kuelekea kilele cha Malkia wa Nguvu 2025 inayoratibiwa na Chombo cha Clouds.

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umewafikia Malkia na Balkia katika Soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa elimu, kuandikisha wanachama wapya waliojiajiri ili waweze kujiunga na kujiwekea akiba kwa kuchangia shilingi 30,000 au zaidi kwa kutoa kidogo kidogo kwa siku bukubuku, wiki, mwezi au msimu kulingana na kipato chake na hapo baadae wote watakuwa wanufaika ws mafao yote yanayotolewa na NSSF yakiwemo ya uzee, uzazi na matibabu.

Akizungumza katika kipindi cha Leo Tena kinachorushwa hewani na kituo cha redio cha Clouds Fm,  Bw. Shabani Mbwana, Afisa Matelekezo Mkuu wa NSSF, amesema lengo la kuanzishwa kwa Mfuko ni kuhakikisha wananchi wanapata kinga dhidi ya majanga kama uzee au kupungua kwa kipato ambapo mtu anayejiwekea akiba anapopatwa na majanga ya aina hiyo atanufaika na mafao kutoka NSSF. Aidha, amesema kuwa Mfuko umeanzisha Skimu maalumu kwa ajili ya wananchi waliojiajiri hivyo amewataka kujiunga na kuchangia ili wawe Mastaa wa Mchezo pale watakaposhindwa kufanya kazi za uzalishaji mali waweze kunufaika na mafao na huduma nyingine zinazotolewa NSSF.












Rais Samia akutana na kuzungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa Bodi ya Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA)




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

 Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye 

mazungumzo na viongozi pamoja na wajumbe wa 

 Bodi ya Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi 

Zanzibar (ZEEA) Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Machi, 2025. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia
 Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na viongozi pamoja
 na wajumbe wa  Bodi ya Wakala wa Uwezeshaji 
Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) Ikulu Jijini
 Dar es Salaam tarehe 26 Machi, 2025.


Rais Samia apokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Félix Tshisekedi Ikulu Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan 
akiwa kwenye mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya
 Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Félix Antoine Tshisekedi ambaye ni
 Waziri wa Mambo ya Nje ya Nchi hiyo Mhe. Thérèse Kayikwamba Wagner, 
Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Machi, 2025.

DAWASA YAPEWA SIKU 90 KUTATUA CHANGAMOTO YA MAZINGIRA FUKWE YA DENGU


Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)

 imepewa siku 90 kuhakikisha adha ya uchafuzi wa

 mazingira inayosababishwa na uunganishaji wa

 mifumo ya maji kiholela fukwe ya Dengu na Fukwe ya Barabara ya

 Obama jirani na 

Hospitali ya Aghakan jijini Dar es Salaam inatatuliwa.

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 26 Machi, 2024 na Naibu Katibu Mkuu ofisi ya 

Makamu wa Rais (Mazingira) Bi. Christina Mndeme alipokuwa akiongea na 

Waandishi wa Habari katika ziara yake iliyohudhuriwa pia na Baraza la Taifa 

la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) la kuhakikisha DAWASA

 wanajenga eneo la kutibu maji kabla ya kuingia baharini ili kulinda Afya ya 

viumbe wa baharini na Ikolojia ya bahari kwa ujumla.


RAIS SAMIA ATENGUA UTEUZI WA DC MASASI! MOBHARE MATINYI APEWA UBALOZI SWEDEN


MKURUGENZI MKUU NSSF AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA

MKURUGENZI MKUU NSSF AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA

Na Mwandishi Wetu,

Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. Masha Mshomba, tarehe 27 Januari 2025 amekutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Robinah Nabbanja Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kikao, Bw. Mshomba amesema Mhe. Robinah Nabbanja amefika nchini kwa lengo kuhudhuria Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika ambapo mbali na mkutano huo aliona ni vizuri kukutana na NSSF kwa lengo la kufahamu mambo kadhaa kuhusu utendaji wa Mfuko ikiwa pamoja na suala la ukuaji wa thamani ya Mfuko, uwekezaji, usajili wa wanachama wa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi na ulipaji wa mafao ya wanachama ili kupata uzoefu.

“Kama tunavyofahamu nchi yetu ya Tanzania imepata heshima kubwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda amefika hapa nchini kwa lengo la kuhudhuria mkutano huo, lakini ameona ni vizuri kuja kukutana na NSSF kwa lengo la kufahamu masuala kadhaa ya utendaji ikiwemo uwekezaji unaofanywa na NSSF, ulipaji wa mafao na masuala mengine ya huduma ikiwemo ushirikiano kati ya NSSF Tanzania na ile ya Uganda' na kwa kweli tumezungumzia hayo ambayo aliomba tuyazungumzie na tumemueleza kwa mfano uwekezaji wetu katika dhamana za Serikali, uwekezaji kwenye miundombinu mfano wa Daraja la Nyerere Kigamboni, Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi kule Morogoro na miradi mengine ambayo NSSF imewekeza ikiwa ni pamoja na ile ya majengo” alisema Bw. Mshomba.

Bw. Mshomba pia alimueleza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda kuwa NSSF ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, hususani kitengo cha Hifadhi ya Jamii pamoja na Benki Kuu ya Tanzania na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwenye masuala ya uwekezaji.

Vile vile, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeimarika sana katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipoingia madarakani.

“Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, NSSF imepata mafanikio makubwa ya utendaji hii inatokana na juhudi kubwa sana ya serikali yake katika kuvutia wawekezaji nchini," alisema Bw. Mshomba.

Alisema kwa sababu NSSF inawafikia waajiri na wajiriwa katika sekta binafsi na pia sekta isiyo rasmi, hivyo wawekezaji wanavyokuja nchini, inapelekea ongezeko la wanachama, inaongeza waajiri, na hivyo kuongeza michango. Aidha, uwekezaji na mapato yanayotokana na uwekezaji yamekuwa yakiongezeka.

Bw. Mshomba alimueleza Mhe. Robinah Nabbanja kuwa NSSF imeruhusiwa kuwekeza nje ya nchi katika eneo la Afrika Mashariki, pia katika eneo la SADC, ambapo kwa uwekezaji huo utasaidia kuongeza mapato ya NSSF kupitia uwekezaji huo.

“Katika uwekezaji huo tulioruhusiwa kuwekeza nje ya nchi, NSSF tumekuwa tukishirikina na Mifuko mingine ya Hifadhi ya Jamii, mfano wenzetu wa NSSF Uganda tunapofikiria kuwekeza katika HISA nchini Uganda ni lazima tushirikiane nao kupata uzoefu wao katika soko la HISA la Uganda," alisema Bw. Mshomba.

Kwa upande wa ushirikiano katika ya Mifuko miwili ya NSSF Tanzania na NSSF Uganda ni mzuri kwani NSSF Tanzania imekuwa ikiwapa ushirikiano mzuri NSSF Uganda hasa wanapokuja kuwekeza Tanzania, ambapo wao wameanza kuwekeza katika dhamana za Serikali kwa muda mrefu.

“ Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda amefurahi sana kuona ushirikiano uliopo na wenzetu wa NSSF  Uganda na akatoa rai kuwa ni vizuri tukaendeleza ushirikiano huo kwa sababu si tu unajenga hizi taasisi mbili bali unajenga nchi na unaimarisha uhusiano katika nchi na nchi kitu ambacho ni muhimu hasa tunapofikiria kuendeleza Jumuiya ya Afrika Mashariki na hilo amesisitiza sana na akaahidi atakaporudi nchini Uganda ataweka msisitizo katika hilo.” aliongeza Bw. Mshomba

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Robinah Nabbanja aliipongeza NSSF kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuwahudumia wanachama na Taifa kwa ujumla na kuomba ushirikiano uendelee kwa maslahi mapana ya nchi zote mbili.





 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa