Serikali yakutana na Mjumbe Malaam wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola
SERIKALI KUFUNGUA FURSA ZA AJIRA KUPITIA MIKATABA MITANO
Serikali Kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano imesaini Mikataba Mitano ambayo itawawezesha wananchi kupata ajira Nje ya Nchi.
Hayo yamesemwa Februari 7, 2026 Jijini Dar es salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu wakati wa Hafla ya Chakula cha Jioni (Gala Dinner) kilichohusisha uzinduzi rasmi wa kipindi cha Imbeju- Bongo Fursa na Jarida la Mapitio ya Vijana lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Biashara na Maendeleo.
“Nlikuwa Falme za Kiarabu nimekutana na Mawaziri wa Kazi kutoka Nchi Mbalimbali na wote walionyesha nia nzuri na nchi yetu, hadi sasa tumesaini Mikataba mitano ambayo iko tayari yamashirikiano na nchi hizi kwa ajili ya Fursa za Ajira kwa Vijana” amesema.
Aidha Mhe. Sangu amesema fursa zilizotajwa kwenye Dira ya Taifa zinapatikana kupitia Wizara hiyo na Serikali inafanya mazungumzo ya mwisho kwenye Mikataba 16 ya Ajira kwa ajili ya Watanzania.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa NEDC, Jesse Madauda Amesema lengo la Jarida na Kipindi chicho ni kuwatia Moyo vijana na Kuwafikia wawekezaji ili waone vijana wa Kitanzania wanafanya shughuli za kibunifu na hatua walizofikia ili iwe rahisi kuwafikia wajasiriamali hao.
Awali akizungumza Mmoja wa Wajasiriamali Elizabeth Consoli ameishukuru serikali kwa kuwa pamoja na wajasiriamali wavumbuzi na kuonyesha nia ya kuwavusha wajasiriamali hao kutoka hatua Moja kwenda Hatua nyengine.
Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni awasili Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 07 Februari, 2026. 

FURSA AJIRA QATAR ZAVUTIA VIJANA WENGI
IAEA yajionea mageuzi ya utoaji huduma katika Taasisi ya Ocean Road
Serikali Yasajili Anwani za Makazi Milioni 12.9
Na Timothy Mwakyenda- MAELEZO
Serikali imesajili zaidi ya Anwani za Makazi Milioni 12.9 ili kuyatambua maeneo mbalimbali na kuyarasimisha kwenye mfumo wa kidijitali.
Takwimu hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Nicholas Merinyo Mkapa kwa niaba ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Bw. Mohamed Hamis Abdullah leo Februari 6, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere kilichopo jijini Dar es salaam ikiwa ni mwendelezo wa Kongamano la Anwani za Makazi na Maonesho ya Teknolojia ya Huduma za Posta.
"Tanzania ilianza mchakato wa usajili wa Anwani za Makazi nchi nzima tangu mwaka 2010, hadi kufikia mwaka 2026 imefanikiwa kusajili zaidi ya anwani milioni 12.9", amesema Naibu Katibu Mkuu, Mkapa.
Naibu Katibu Mkuu Mkapa ameongeza kuwa, Anwani za Makazi ni kitovu cha maendeleo kwa nchi kwa sababu zinatambua na kuunganisha maeneo mbalimbali ya nchi na kuziweka pamoja katika mfumo wa kidijitali ambapo toka zoezi la usajili lianze, jumla ya mifumo 29 imeunganishwa ikiwemo Shirika la Posta.
Ametoa rai kwa washiriki wa kongamano hilo kuwa katika siku za majadiliano, wajumbe waweke mkazo katika kujadili namna ambavyo Anwani za Makazi zina umuhimu katika utoaji wa huduma za afya, elimu na kukuza uchumi.
Aidha, Mkapa amesisitiza kuwa mifumo imara ya Anwani za Makazi huimarisha utu wa watu na kuibua fursa za kimaendeleo kwa watu wote.
MHE. DKT SAMIA AREJEA TANZANIA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wakati akitokea Dubai, tarehe 6 Februari, 2026. alipokuwa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Mhe. Rais Dkt. Samia alishiriki katika Mkutano wa Dunia wa Serikali (World Governments Summit – WGS) 2026 pamoja na Uzinduzi wa Jukwaa la Kimataifa wa Uwekezaji Afrika (GAIS).
___
#TanzaniaNaUwekezaji
#DiplomasiaYaKiuchumi
#KaziNaUtuTunasongaMbele
RAIS DKT SAMIA KUZINDUA SOKO LA KARIAKOO FEBRUARI 08, 2026
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan anatarajia kuzindua soko la Kariakoo Februari 8, 2026 ambalo lilikuwa kwenye ukarabati baada ya kuungua na moto na Soko jipya ambalo limejengwa
Akizungumzia ujio wa Rais Dkt Samia RC Chalamila amesema soko hilo kwa sasa limekamilika kwa asilimia 100 ambapo zaidi ya shilingi bilioni 28 zimetumika kukarabati na kujenga soko jipya likiwa na takribani vizimba zaidi ya 1500 kwa ajili ya wafanyabiashara
RC Chalamila amewataka wananchi wakazi wa Mkoa huo, wafanyabiashara wadogo wa kati na wakubwa kujitokeza kwenye uzinduzi huo wa Soko la kariakoo ili kumuunga mkono Rais Dokta Samia lakini pia kuweka historia ya tukio hilo kubwa linalotarajiwa kuwa ni kiungo muhimu katika kujenga uchumi wa Mkoa huo na Taifa kwa ujumla
Aidha Chalamila ameagiza wafanyabiashara wadogo ambao wamefunga barabara za kuingia soko la kariakoo waondoke na waache barabara hizo wazi kabla ya februari 8 ili kuruhusu wafanyabiashara kuingia kwenye Soko hilo.
Wanawake wametakiwa kuzingatia uvaaji wa viatu vyenye kisigino kifupi
Wanawake wametakiwa kuzingatia uvaaji wa viatu vyenye kisigino kifupi kuimarisha afya ya miguu na kuepuka kuvaa viatu vyenye kisigino kirefu ama kisigino flati ambavyo ni hatari kwa afya ya magoti.
Akizungumza na wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) kanda ya Mabibo katika kambi ya matibabu ya siku mbili ya uchunguzi wa afya Mtaalamu wa mazoezi tiba kutoka JKCI Jaqline Mariki alisema mtu anatakiwa kuvaa viatu vyenye kisigino kifupi ili unyayo uweze kunyanyuka kidogo kusaidia ugawanyishwaji wa uzito kwenye mwili hivyo kutoleta maumivu katika mwili.
MALKIA NA BALKIA WACHANGAMKIA FURSA YA KUJIWEKEA AKIBA NA NSSF
Katika kuelekea kilele cha Malkia wa Nguvu 2025 inayoratibiwa na Chombo cha Clouds.
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umewafikia Malkia na Balkia katika Soko la Kariakoo, jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa elimu, kuandikisha wanachama wapya waliojiajiri ili waweze kujiunga na kujiwekea akiba kwa kuchangia shilingi 30,000 au zaidi kwa kutoa kidogo kidogo kwa siku bukubuku, wiki, mwezi au msimu kulingana na kipato chake na hapo baadae wote watakuwa wanufaika ws mafao yote yanayotolewa na NSSF yakiwemo ya uzee, uzazi na matibabu.
Akizungumza katika kipindi cha Leo Tena kinachorushwa hewani na kituo cha redio cha Clouds Fm, Bw. Shabani Mbwana, Afisa Matelekezo Mkuu wa NSSF, amesema lengo la kuanzishwa kwa Mfuko ni kuhakikisha wananchi wanapata kinga dhidi ya majanga kama uzee au kupungua kwa kipato ambapo mtu anayejiwekea akiba anapopatwa na majanga ya aina hiyo atanufaika na mafao kutoka NSSF. Aidha, amesema kuwa Mfuko umeanzisha Skimu maalumu kwa ajili ya wananchi waliojiajiri hivyo amewataka kujiunga na kuchangia ili wawe Mastaa wa Mchezo pale watakaposhindwa kufanya kazi za uzalishaji mali waweze kunufaika na mafao na huduma nyingine zinazotolewa NSSF.
Rais Samia akutana na kuzungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa Bodi ya Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye
mazungumzo na viongozi pamoja na wajumbe wa
Bodi ya Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi
Zanzibar (ZEEA) Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Machi, 2025.
Rais Samia apokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. Félix Tshisekedi Ikulu Jijini Dar es Salaam
DAWASA YAPEWA SIKU 90 KUTATUA CHANGAMOTO YA MAZINGIRA FUKWE YA DENGU
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)
imepewa siku 90 kuhakikisha adha ya uchafuzi wa
mazingira inayosababishwa na uunganishaji wa
mifumo ya maji kiholela fukwe ya Dengu na Fukwe ya Barabara ya
Obama jirani na
Makamu wa Rais (Mazingira) Bi. Christina Mndeme alipokuwa akiongea na
Waandishi wa Habari katika ziara yake iliyohudhuriwa pia na Baraza la Taifa
la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) la kuhakikisha DAWASA
wanajenga eneo la kutibu maji kabla ya kuingia baharini ili kulinda Afya ya
MKURUGENZI MKUU NSSF AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA
MKURUGENZI MKUU NSSF AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA UGANDA
Na Mwandishi Wetu,
Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. Masha Mshomba, tarehe 27 Januari 2025 amekutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Robinah Nabbanja Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya kikao, Bw. Mshomba amesema Mhe. Robinah Nabbanja amefika nchini kwa lengo kuhudhuria Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika ambapo mbali na mkutano huo aliona ni vizuri kukutana na NSSF kwa lengo la kufahamu mambo kadhaa kuhusu utendaji wa Mfuko ikiwa pamoja na suala la ukuaji wa thamani ya Mfuko, uwekezaji, usajili wa wanachama wa sekta binafsi na sekta isiyo rasmi na ulipaji wa mafao ya wanachama ili kupata uzoefu.
“Kama tunavyofahamu nchi yetu ya Tanzania imepata heshima kubwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkubwa wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda amefika hapa nchini kwa lengo la kuhudhuria mkutano huo, lakini ameona ni vizuri kuja kukutana na NSSF kwa lengo la kufahamu masuala kadhaa ya utendaji ikiwemo uwekezaji unaofanywa na NSSF, ulipaji wa mafao na masuala mengine ya huduma ikiwemo ushirikiano kati ya NSSF Tanzania na ile ya Uganda' na kwa kweli tumezungumzia hayo ambayo aliomba tuyazungumzie na tumemueleza kwa mfano uwekezaji wetu katika dhamana za Serikali, uwekezaji kwenye miundombinu mfano wa Daraja la Nyerere Kigamboni, Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi kule Morogoro na miradi mengine ambayo NSSF imewekeza ikiwa ni pamoja na ile ya majengo” alisema Bw. Mshomba.
Bw. Mshomba pia alimueleza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda kuwa NSSF ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, hususani kitengo cha Hifadhi ya Jamii pamoja na Benki Kuu ya Tanzania na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwenye masuala ya uwekezaji.
Vile vile, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeimarika sana katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipoingia madarakani.
“Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, NSSF imepata mafanikio makubwa ya utendaji hii inatokana na juhudi kubwa sana ya serikali yake katika kuvutia wawekezaji nchini," alisema Bw. Mshomba.
Alisema kwa sababu NSSF inawafikia waajiri na wajiriwa katika sekta binafsi na pia sekta isiyo rasmi, hivyo wawekezaji wanavyokuja nchini, inapelekea ongezeko la wanachama, inaongeza waajiri, na hivyo kuongeza michango. Aidha, uwekezaji na mapato yanayotokana na uwekezaji yamekuwa yakiongezeka.
Bw. Mshomba alimueleza Mhe. Robinah Nabbanja kuwa NSSF imeruhusiwa kuwekeza nje ya nchi katika eneo la Afrika Mashariki, pia katika eneo la SADC, ambapo kwa uwekezaji huo utasaidia kuongeza mapato ya NSSF kupitia uwekezaji huo.
“Katika uwekezaji huo tulioruhusiwa kuwekeza nje ya nchi, NSSF tumekuwa tukishirikina na Mifuko mingine ya Hifadhi ya Jamii, mfano wenzetu wa NSSF Uganda tunapofikiria kuwekeza katika HISA nchini Uganda ni lazima tushirikiane nao kupata uzoefu wao katika soko la HISA la Uganda," alisema Bw. Mshomba.
Kwa upande wa ushirikiano katika ya Mifuko miwili ya NSSF Tanzania na NSSF Uganda ni mzuri kwani NSSF Tanzania imekuwa ikiwapa ushirikiano mzuri NSSF Uganda hasa wanapokuja kuwekeza Tanzania, ambapo wao wameanza kuwekeza katika dhamana za Serikali kwa muda mrefu.
“ Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda amefurahi sana kuona ushirikiano uliopo na wenzetu wa NSSF Uganda na akatoa rai kuwa ni vizuri tukaendeleza ushirikiano huo kwa sababu si tu unajenga hizi taasisi mbili bali unajenga nchi na unaimarisha uhusiano katika nchi na nchi kitu ambacho ni muhimu hasa tunapofikiria kuendeleza Jumuiya ya Afrika Mashariki na hilo amesisitiza sana na akaahidi atakaporudi nchini Uganda ataweka msisitizo katika hilo.” aliongeza Bw. Mshomba
Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Robinah Nabbanja aliipongeza NSSF kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuwahudumia wanachama na Taifa kwa ujumla na kuomba ushirikiano uendelee kwa maslahi mapana ya nchi zote mbili.


.jpeg)





%20NSSF.jpg)



















.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)












.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
