Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

KWESE FREE SPORTS TANZANIA (TV1) NA TBC KUONESHA BURE, MUBASHARA 'LIVE' KOMBE LA DUNIA (2018), BILA KULIPIA KING'AMUZI

KFS Tanzania imetangaza rasmi leo kuwa ndio kituo pekee nchini kitakachorusha matangazo ya michuano ya Kombe la Dunia 2018 (FiFA World Cup 2018) bure inayotarajiwa kuanza tarehe 14 Juni 2018 na kumalizika tarehe 15 Julai 2018 nchini Urusi. 

KFS Tanzania wakishirikiana na kituo cha Televisheni cha TBC watarusha matangazo hayo moja kwa moja.
Kutakuwa na mechi 32 zikiwemo zote zitakazochezwa na timu za Afrika, Robo Fainali, Nusu Fainali pamoja na Mechi za mwisho ya Fainali,hii si ya kuikosa hata kidogo.

KFS inapatikana kupitia King'amuzi cha Startimes Chanel 103, Continental Chanel namba 07 na Ting Chanel namba 36
Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayub Rioba(Kulia) akisaini Mkataba wa makubaliano kati ya KWESE free Sports (TV1) na TBC kuonesha Kombe la Dunia kuanzia Juni 14,2018
Mkurugenzi wa KWESE free Sports (TV1) Bw. Joseph Sayi(kushoto) akisaini Mkataba wa makubaliano kati ya KWESE free Sports (TV1) na TBC kuonesha Kombe la Dunia  kuanzia Juni 14,2018
Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayub Rioba pamoja na Mkurugenzi wa KWESE Free Sports Tanzania (TV1) Bw. Joseph Sayi wakipeana Mikono baada ya kusaini mkataba wa makubaliano kuonesha Mubashara Kombe la Dunia 2018, Buree bila kulipia.
Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayub Rioba pamoja na Mkurugenzi wa KWESE Free Sports Tanzania (TV1) Bw. Joseph Sayi wakionesha waandishi wa Habari Mkataba waliosaini kushirikiana kuonesha Kombe la Dunia 2018.
Mkurugenzi Mkuu wa TBC Dkt. Ayub Rioba akitoa neno wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari baada ya kuasini mkataba kati ya KWESE Free Sport Tanzania(TV1) na TBC kuonesha Kombe la Dunia mwaka 2018
Mkurugenzi wa KWESE Free Sport Tanzania(TV1) Bw. Joseph Sayi  akitoa neno wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari baada ya kuasini mkataba kati ya KWESE Free Sport Tanzania(TV1) na TBC kuonesha Kombe la Dunia mwaka 2018
Meneja Masoko wa TBC Bi. Daphrosa Kimbory akiwasisitiza wafanyabiashara na watu mbalimbali kutumia fursa ya Kombe la Dunia kujitangaza na kuonesha bidhaa mbalimbali wakati wa kurushwa moja kwa moja kwa mashindano ya Kombe la Dunia 2018 (FIFA World Cup 2018)
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TBC Bi. Edna Rajabu akiongea na waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa kampeni za urushaji mechi kombe la Dunia 2018
Meneja Masoko wa KWESE Free Sport Tanzania(TV1) Bi. Gillian Rugumamu, akiwahakikishia watanzania kuwa KWESE Free Sport Tanzania (TV1) pamoja na TBC watawaletea Burudani ya Kombe la Dunia Mubashara tena Buree na kwa Kiswahili hivyo waondoe wasi wasi wa kuwaza kulipia King'amuzi maana kutakuwa hakuna makato yoyote.
Mbunifu na Uzalishaji wa Vipindi kutoka KWESE Free Sport Tanzania(TV1) Bw. Walter, akiwahakikishia watananzania kuwa kutakuwa na Studio mahili za utangazaji zenye watu mahili ambao watachambua Mechi zote za Kombe la Dunia 2018, hatua kwa hatua na kurushwa Mubashara bila Chenga.
Meneja Mkuu  wa KWESE Free Sport Tanzania(TV1) Bw. Mgope Kiwanga akizungumza neno wakati wa Mkutano na waandishi wa Habari 
Mhariri wa vipindi vya Michezo kutoka TBC Bw. Enock Mbwigane akitoa neno baada ya kumaliza mkutano pamoja na waandishi wa Habari
Wanahabari na wadau mbalimbali wa Michezo wakiwa katika Mkutano.
Picha na Blogs za Mikoa Tanzania.

JUMIA FIX MY HOUSE.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

It's time to turn your House to a HOME!!

A house can be any basic unit of dwelling, whether its an apartment, a super modern glass box or anything else in between. The form of the house never matters as much as what goes inside  because those are the special things that transform any space into a home.

What's the difference between a house and a home? A house is a structure that provides you basic needs and safety. A home is a place that provides you mental and emotional support, a place you look forward to being in to get away from the outside world.

Feeling like your home is lacking a bit of personality? There’s something powerful about walking into a house that feels like a home and reflects the owner’s personality so perfectly. Do you feel that way about your house? If not? Do you wish to achieve a high-end luxurious look without blowing your budget? Believe it or not, your home can look expensive and luxurious without dragging you into debt.The key is to shop SMART..

One of the wonderful experience i had this weekend as i spend some time alone on my internet was to  bump into one of the Upcoming Jumia’s Campaign. The name made me look and look again,They call it Big Home Makeover!! Fascinating right?

An online survey released by Jumia Tanzania has revealed that 70% of Tanzanians households keep their home appliances for more than their life span citing sentimental value and uniqueness as opposed to old age.

“Large home appliances like dishwashers, microwaves, washing machines , refrigerators and furniture have an average lifespan of up to 10 years. They are a major investment for customers, and therefore people look for brands that will last. It is quite surprising  to discover quite how long they keep them though! The survey showed that people keep them as long as possible - often up to 10 years or more”, said Jumia Head of Home and Living Appliances, Priscilla Eliphas.

I was impressed because at least Jumia Tanzania understands that a house makeover can be an expensive task, That is why they brought us Home Lovers  a whole week of  shopping for the best prices on home essentials like appliances, kitchen and dining, home decor, dishwashers, washers and dryers, fridges and freezers, ironing and laundry etc, from April 16th-26th.

We, Home Lovers have to get ready for a week of the largest discounts as Jumia continues to partner with trusted brands to sell quality and affordable home appliances and offer up to 20,0000 assortment to choose from thus people do not need to hold to home appliances for longer than necessary”, Brands such as Samsung, Bruhm,Geepas, Nippotec, TCL, Star X, Philips, Aborder, Nikai, Ocean and Tronic.  They will also have some special surprises in the lead up to the event such as give aways, treasure hunts on their website, shopping vouchers etc,I personally can't wait!

Jumia is an online Marketplace that provides sellers and buyers the most convenient shopping and selling experience . A Platform for vendors to display and sell their products directly to consumers and for buyers to have a wide range of products to choose from with the best prices in the market. Jumia Tanzania provides a solution for everything you need, at the best price, with convenient home delivery with a very simple process.
Browse the website for the product you need, add it to your online basket, then checkout and leave your details, and Jumia will deliver to your door.

Top  Reasons You Should shop during Home Makeover

     Time to replace those old sufurias, mattresses, cookers, sofas, etc! save the date: 16th-26th April
     Treat your house to a sparkling home makeover by simply - Pendezesha Nyumba na Jumia
     No hustle and bustles of shopping! - Pay cash on delivery all from the comfort of your home! How cool, right?
     Enjoy the shortest delivery time on Jumia
     Unbeatable Prices
     Flash Sales – Get amazing deals on TV’s, cookers and mattresses during the campaign
     Voucher Discounts-Shopping has never been so much fun! Get voucher discounts to enjoy your shopping  for less!
     Over 20,000 assortment to choose from! Spoilt for choice with discounts of up to 60% off!


KATIBU MKUU NISHATI, AKUTANA NA WADAU WA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua ( kulia) akiongoza kikao kilichokutanisha wadau wa maendeleo na Wizara ya Nishati katika Ofisi za Wizara ya Nishati jijini Dar es Salaam tarehe 06 Aprili, 2017.
Sehemu ya washiriki wa kikao hicho wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani)

Wataalam wa Idara ya Nishati, wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani)

TAMKO LA SERIKALI KUHUSU WATUMISHI WALIIONDOLEWA KWENYE MFUMO WA MALIPO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI KWA KIPINDI CHA JANUARI HADI MACHI 2018

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


TAARIFA KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI KWA KIPINDI CHA JANUARI HADI MACHI 2018 ILIYOTOLEWA NA MHE. UMMY MWALIMU (MB); WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, TAREHE 9 APRILI, 2018.

Ndugu Wanahabari,
Serikali kupitia Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto imekuwa ikitoa taarifa ya mwenendo wa mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu na hatua zinazochukuliwa kudhibiti ugonjwa huu Kuanzia Januari hadi kufikia tarehe 31 Machi 2018, jumla ya wagonjwa 1448, wametolewa taarifa, na kati ya hao 27 wamepoteza maisha.

Kwa kipindi cha Januari wagonjwa 365 na vifo 9 walitolewa taarifa, Februari wagonjwa 996 na vifo 18 na Machi wagonjwa 87 bila kifo. Mwenendo wa takwimu hizi za ugonjwa wa Kipindupindu zinaonyesha kuwa idadi ya wagonjwa na vifo imepungua kwa kiasi kikubwa. Aidha, Mkoa wa Dodoma umeongoza kwa kipindi cha Januari hadi Machi kwa kuripoti jumla ya wagonjwa 583 kati ya 1,448 walioripotiwa nchi nzima sawa na asilimia 40.3%, ikifuatiwa na Ruvuma 374 (25.8%), Rukwa 276 (19.1%), Iringa 88 (6.1%), Morogoro 56 (3.9%), Songwe 37 (2.6%), Kigoma 25 (1.7%) na Manyara 9 (0.6%).

Kwa mwezi Machi 2018, jumla ya wagonjwa 87 bila kifo wametolewa taarifa, ambapo ni pungufu kubwa sawa na asilimia 91.3% ukilinganisha na mwezi Februari 2018 ambapo kulikuwa na jumla ya wagonjwa 996 na vifo 18. Kwa mwezi Machi mikoa na halmashauri ambazo zimeendelea kutoa taarifa ya ugonjwa wa Kipindupindu nchini ni Dodoma (Mpwapwa-35, Chamwino-15, Dodoma Mjini-6, Kongwa-5), Ruvuma (Nyasa-18, Mbinga-5), Rukwa (Sumbawanga Vijijini-5), na Iringa (Kilolo-2).

Ukilinganisha idadi ya wagonjwa waliotolewa taarifa mwezi Februari na ule wa mwezi Machi, mikoa imeweza kufanikiwa kudhibiti ugonjwa huu kwa kiasi kikubwa. Mfano mkoa wa Morogoro umefanikiwa kudhibiti kikamilifu kutoka wagonjwa 56 mwezi Februari na kutokuwa na wagonjwa wowote mwezi Machi. Mikoa mingine iliyofanikiwa kupunguza idadi ya wagonjwa kwa sehemu kubwa katika kipindi cha mwezi mmoja ni Iringa (punguzo la asilimia 97.7%), Rukwa (punguzo la asilimia 96.1%) na Ruvuma (punguzo la asilimia 92.7%). Mkoa wa Dodoma pia umefanikiwa kupunguza idadi ya wagonjwa kwa takribani asilimia 83% katika kipindi cha mwezi mmoja.

Wizara inatoa pongezi kwa Mikoa kwa jitihada mbalimbali walizozichukuwa kudhibiti ugonjwa huo ambayo imepelekea kupunguza kwa sehemu kubwa kuenea kwa ugonjwa huu katika kipindi cha mwezi wa Machi.

Ndugu Wanahabari,
Ingawa takwimu hizi zinaonyesha kuwa ugonjwa umepungua, bado uwezekano wa kuenea kwa ugonjwa wa Kipindupindu na kupata maambukizi mapya ni tishio hata kama ni Halmashauri moja tu itakuwa na wagonjwa wa Kipindupindu. Tishio hili inaongezeka katika msimu huu wa mvua ambapo inaweza kuongeza kasi ya kuenea kwa maambukizi ya Kipindupindu. Hivyo tunahitaji kuzidisha juhudi za kuzuia ugonjwa huu, kwa kusimamia kikamilifu maelekezo na miongozo stahiki inayotolewa. 

Ni dhahiri kuwa ushirikishwaji wa sekta zote kwa ngazi mbalimbali na jamii kwa ujumla ni muhimu sana katika kukabiliana na ugonjwa wa Kipindupindu.  Wizara inasisitiza kuwa wadau wote wapewe nafasi katika mapambano haya kupitia vikao mbalimbali za kujadili udhibiti wa ugonjwa wa Kipindupindu kwenye Halmashauri na Mikoa. Viongozi wa dini, watu mashuhuri na waganga wa tiba mbadala pia wasaidie kuhamasisha jamii zao kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huu.

Ndugu Wanahabari,
Wizara inaendelea kuwasihi wananchi kuungana na Halmashauri, Mikoa, hasa iliyotoa taarifa kipindi cha Januari hadi Machi, pamoja na Wizara katika juhudi za kupambana na kuenea kwa ugonjwa wa Kipindupindu.  Jamii izingatie kanuni za usafi binafsi na usafi wa mazingira, ikiwa ni pamoja na:
1.   Kujenga na kutumia vyoo bora katika maeneo tunayoishi.
2.   Kunawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni kabla ya kula, baada ya kutumia choo, na baada ya kumsafisha mtoto aliyejisaidia.
3.   Kunywa maji safi na salama yaliyotakaswa kwa dawa (kama vile water guard) au yaliyochemshwa na kupoa.
4.   Kuzingatia ushauri na elimu sahihi kuhusu ugonjwa wa Kipindupindu, ili jamii iondokane na imani potofu kuhusu Kipindupindu.
5.   Kufikisha wagonjwa wa Kipindupindu mapema katika vituo vya kutolea huduma ili wawahi kupata matibabu.
6.   Kutotiririsha maji   taka   ovyo

Vile vile, Wizara inasisitiza yafuatayo yasimamiwe kwenye Halmashauri na Mikoa yote nchini,
1.   Utoaji wa taarifa sahihi za ugonjwa wa Kipindupindu na kwa wakati kwa kufuata miongozo iliyopo.
2.   Usimamizi wa utekelezaji wa miongozo katika kuzuia na kudhibiti ugonjwa ni pamoja na;
o   Usimamizi wa utekelezaji wa sheria ndogondodo za usafi wa mazingira ili kuimarisha matumizi ya vyoo.
o   Usafi wa mazingira pamoja na udhibiti wa biashara za chakula na pombe za kienyeji katika mitaa.
o   Kuzingatia agizo la Mheshimiwa Rais la kufanya usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi.
3.   Kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yote mijini na vijijini hasa wakati wa mlipuko wa Kipindupindu. Hii ni pamoja na:
o   Mamlaka za maji katika ngazi zote ziweke mkazo wa kuwepo kwa vyanzo mbadala vya maji.
o   Utakasaji wa maji ya bomba kwa njia ya kutumia klorini ufanyike kama miongozo inavyotaka na ufuatiliaji wa ubora wa maji ufanyike kulingana na miongozo.

Hitimisho
Wizara kwa ukaribu itaendelea kufuatilia mwenendo wa ugonjwa wa Kipindupindu nchi nzima. Aidha, Wizara inawashukuru wadau wote wa sekta mbalimbali, wataalamu na watumishi, waandishi wa habari na wananchi kwa michango yao mbalimbali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kipindupindu nchini.  


Asanteni sana

Wateja 676 wa Tigo wajinyakulia simu janja za TECNO R6 na bonasi za intaneti bure baada ya kununua bando za intaneti kupitia *147*00#

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (kushoto) na Mtalaam wa Bidhaa wa Tigo,  Jacqueline Nnunduma (kulia) wakiongea na waandishi wa habari katika hafla ya kukabidhi zawadi za simu janja aina ya Tecno R6 kwa washindi wa promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#. 


Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (aliyesimama kulia) akimkabidhi Gladness Mori (alieyeketi)
zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus huku akitazamwa na baadhi ya washindi wengine wa promosheni hiyo. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#. 


Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (aliyesimama kulia) akimkabidhi Diana Pumpuni  zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus huku akitazamwa na baadhi ya washindi wengine wa promosheni hiyo. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#. 

Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael (aliyesimama kulia) akimkabidhi Charles Shabani  zawadi ya simu janja aina ya Tecno R6 aliyoshinda katika promosheni inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus huku akitazamwa na baadhi ya washindi wengine wa promosheni hiyo. Tigo imetoa jumla ya simu 676 bure pamoja na bonasi za intaneti hadi GB 1 kwa wateja wake walionunua bando za intaneti kupitia menu yake iliyoboreshwa ya *147*00#. 

Nyaka Nyaka Bonus - Promosheni ya Tigo Inayoongeza Matumizi ya Intaneti Nchini

  • Zaidi ya simu 400 na bonasi za intaneti bado zinashindaniwa!
Dar es Salaam, Aprili 5, 2018 – Kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali nchini ya Tigo Tanzania inazidi kuongeza idadi ya watumiaji wa huduma za intaneti nchini baada ya kuwazawadia wateja wake 676 simu janja aina ya Tecno R6 katika promosheni yake inayoendelea ya Nyaka Nyaka Bonus.
Katika promosheni hii murwa ambapo Tigo inatoa jumla ya simu janja 12 kila siku, wateja wote wa Tigo wanaonunua bando za intaneti za kuanzia TSH 1,000 kupitia menu iliyoboreshwa ya *147*00# pia wanapata bonasi ya hadi GB 1 bure kwa matumizi ya mitandao ya kijamii ya Facebook, WhatsApp, Instagram na Twitter.

‘Ofa hii kabambe ni sehemu ya ubunifu wa Tigo unaoendana na maslahi na mahitaji ya wateja ili kuwezesha kila mtu kufurahia maisha bora ya kidigitali kupitia mtandao wetu mpana wa Tigo,’ Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael alisema katika hafla fupi ya kuwakabidhi washindi simu zao jijini Dar es Salaam leo.


Akizungumza katika hafla kama hiyo iliyofanyika mjini Morogoro leo, Mtalaam wa Usambaji Bidhaa wa Tigo, Baraka Hamza alisema kuwa kupitia promosheni hii ya Nyaka Nyaka Bonus, Tigo inafanikisha azma yake ya kuwaunganisha wananchi wote na mtandao wake wenye kasi ya juu na mpana zaidi nchini wa Tigo 4G.


‘Tunataka kila mtu awe sehemu ya mabadiliko makubwa yanayotokana na kuunganishwa na mtandao wa intaneti na pia kufurahia huduma bora zenye uwezo wa kubadili maisha zinazotopatikana katika mtandao wetu wenye kasi ya juu na mpana zaidi nchini wa Tigo 4G unaopatikana katika miji 24 nchini,’ alisema.


Takwimu za hivi karibuni zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonesha kuwa asilimia 45% tu ya Watanzania ndiyo waliofikiwa na huduma za kimtandao, huku asilimia 84% ya wale waliofikiwa wakitumia simu zao za mkononi kama njia kuu ya kupata huduma hizo za mtandao. Ubunifu huu wa Tigo utahakikisha kuwa idadi ya watumiaji wa huduma za mtandao inaongezeka nchini.


‘Tunawaasa wateja wetu kuchangamkia fursa hii kubwa ya kuwa sehemu ya mageuzi ya ulimwengu wa kisasa wa kidigitali kwa kununua bando intaneti kupitia *147*00# ili wajipatie bonasi za intaneti pamoja na nafasi ya kujishinidia simu janja aina ya Tecno R6 kutoka Tigo.’ Woinde alibainisha.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa