Kaimu
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kiufundi kwa Afrika Gashaw Gebeyehu
Wolde wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA)akizungumza na
waandishi wa habari mara baada ya kutembembelea mashine za kisasa
katika Taasisi ya Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Mtendaji
Mkuu wa Taasisi ya Ocean Road Dkt.Diwani Msemo akizungumza kuhusiana na
mikakati ya Taasisi mara baada ya kutembelewa na IAEA jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Profesa Najat Kassim Mohammed
akizungumza kuhusiana na ujio wa IAEA katika Taasisi ya Ocean Road
kuangalia mashine za miozi, jijini Dar es Salaam.
*Waahidi kuwa wa kwanza kudhibitisha Ithibati ya ubora.
Na Mwandishi Wetu
SHIRIKA
la Kimataifa la Nguvu za Atomiki (IAEA) limesema kuwa Taasisi ya Ocean
Road imefanya mageuzi katika utoaji huduma za saratani.
Akizungumza
katika ziara ya Shirika hilo likiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya
Ushirikiano wa Kiufundi kwa Afrika Gashaw Gebeyehu Wolde amesema Taasisi
ya Ocean Road katika imefanya mageuzi makubwa ya kuwa na vifaa vya
teknolojia katika otoaji wa huduma za Saratani ikilinganishwa na miaka
iliyopita wakati walipotembelea.
Wolde
amesema katika hatua ambayo imefikiwa watakuwa watu kwanza katika
kupitisha ithibati ya ubora ya huduma ya Saratani na kufanya Taasisi ya
Ocean Road kuwa ya Tatu Afrika katika utoaji huduma hiyo.
Amesema
Serikali ya Tanzania imewekeza katika kuwa na miundombinu pamoja na
vifaa vya Kisasa ikiwemo za ugunduzi wa saratani za aina mbalimbali.
Aidha
amesema IAEA itaendelea kutoa ushirikiano kwa Taasisi ya Saratani Ocean
Road (ORCI) ili kuimarisha ushirikiano, ikiwa ni pamoja na mafunzo ya
matumizi ya mashine za CT-Scan na kutoa vifaa vya mionzi na kusomesha
wataalam katika ubobezi wa magonjwa ya saratani.
Hata
hivyo Wolde ametoa shukurani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa
ununuaji wa mashine za kisasa na fedha nyingi katika Taasisi ya Ocean
Road.
Mtendaji
Mkuu wa Taasisi ya Ocean Road Dkt.Diwani Msemo amesema kuwa ujumbe IAEA
wametembelea mashine mbalimbali na kuona Taasisi hiyo imejipanga.
Amesema miundombinu na vifaa tiba vilivyopo vimeongeza huduma katika kutoa huduma kwa mgonjwa bila kuathiri .
Hata hivyo amesema ujumbe huo umekiri kuwa mashine zilizopo za kisasa katika hospitali za Afrika Mashariki.
Mkurugenzi
Mkuu wa Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC) Profesa Najat Kassim Mohammed
amesema Taasisi ya Ocean Road imepiga hatua kubwa katika utoaji wa
huduma ya Saratani.
Aidha
ametoa shukurani kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan katika uwezeshaji wa
vifaa vya kisasa katika Taasisi ya Ocean kwa kutumia Fedha za ndani.



0 comments:
Post a Comment