Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)
imepewa siku 90 kuhakikisha adha ya uchafuzi wa
mazingira inayosababishwa na uunganishaji wa
mifumo ya maji kiholela fukwe ya Dengu na Fukwe ya Barabara ya
Obama jirani na
Hospitali ya Aghakan jijini Dar es Salaam inatatuliwa.
Agizo hilo limetolewa leo tarehe 26 Machi, 2024 na Naibu Katibu Mkuu ofisi ya
Makamu wa Rais (Mazingira) Bi. Christina Mndeme alipokuwa akiongea na
Waandishi wa Habari katika ziara yake iliyohudhuriwa pia na Baraza la Taifa
la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) la kuhakikisha DAWASA
wanajenga eneo la kutibu maji kabla ya kuingia baharini ili kulinda Afya ya
viumbe wa baharini na Ikolojia ya bahari kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment