Home » » DAWASA YAPEWA SIKU 90 KUTATUA CHANGAMOTO YA MAZINGIRA FUKWE YA DENGU

DAWASA YAPEWA SIKU 90 KUTATUA CHANGAMOTO YA MAZINGIRA FUKWE YA DENGU


Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)

 imepewa siku 90 kuhakikisha adha ya uchafuzi wa

 mazingira inayosababishwa na uunganishaji wa

 mifumo ya maji kiholela fukwe ya Dengu na Fukwe ya Barabara ya

 Obama jirani na 

Hospitali ya Aghakan jijini Dar es Salaam inatatuliwa.

Agizo hilo limetolewa leo tarehe 26 Machi, 2024 na Naibu Katibu Mkuu ofisi ya 

Makamu wa Rais (Mazingira) Bi. Christina Mndeme alipokuwa akiongea na 

Waandishi wa Habari katika ziara yake iliyohudhuriwa pia na Baraza la Taifa 

la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) la kuhakikisha DAWASA

 wanajenga eneo la kutibu maji kabla ya kuingia baharini ili kulinda Afya ya 

viumbe wa baharini na Ikolojia ya bahari kwa ujumla.


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa