Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Zawadi Msalla
Chama
Cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) kimeeleza masikitiko yao juu ya ushiriki mbovu
wa Viziwi katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwezi Oktoba kote nchini.
Akizungumza
na waandishi wa Habari katika ukumbi wa Habari-MAELEZO leo Mshauri Mwelekezi wa
Elimu ya Uraia kwa Watu wenye Ulemavu Bw. Novat Rukwago amesema kuwa, licha ya
jitihada mbalimbali ambazo walijaribu kuzifanya ili kuhakikisha viziwi kote
nchini wanapata haki yao ya msingi na ya kikatiba ya kupiga kura bado ushiriki
wao haukuridhisha.
Rukwago
alizitaja changamoto mbalimbali zilizo jitokeza katika uchaguzi huo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa wataalamu wa
lugha za alama zinazotumiwa na viziwi katika kampeni mbalimbali za Vyama vya
Siasa, hivyo sera na Ilani za vyama hivyo hazikuweza kujulikana kwa viziwi.
“Vyama
vingi vilisema ni suala la rasilimali na ukosefu wa fedha za kuweka wataalamu
hao, ingawa tuonavyo sisi ni kwamba walishindwa kutoa kipaumbele na si suala la
fedha,” alisema Rukwago.
Aidha,
Rukwago alisema CHAVITA kwa juhudi binafsi waliweza kutembea jumla ya mikoa 17
kote nchini na kufanikiwa kutoa elimu kwa baadhi ya viziwi ambapo jumla ya
viziwi 2516 walijiandikisha, idadi hiyo ikiwa na wanaume 1256 na wanawake 1260.
Waliopiga kura walikuwa ni 1807.
Aliongeza
kwa kusema kuwa licha ya changamoto hizo pia mazingira ya kupigia kura hayakuwa
rafiki kwa watu wenye uhitaji maalumu kwani hakukuwa na wataalamu wa lugha za
alama katika vituo vya kupigia kura.
Waliiomba
Serikali kuzingatia umuhimu wa kuyapa kipaumbele makundi mbalimbali yenye uhitaji
kwa chaguzi zijazo na kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya mawasiliano na
vyama vya watu wenye uhitaji maalum mapema ili kuweza kushirikiana katika
kuondoa changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi wa mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment