Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Serikali imesema ipo mbioni kufufua kiwanda
cha General Tyres ambacho kilisitisha shughuli zake za uzalishaji kwa
muda mrefu baada ya kumlipa mwekezaji asilimia 26% alizokuwa anaidai
serikali na sasa kiwanda ni cha serikali.
Kauli ya serikali imetolewa bungeni na
waziri viwanda biashara na uwekezaji Charles Mwijage wakati akijibu
swali la mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari (Chadema).
Nassari ametaka kujua kwanini serikali
imekuwa na ahadi zisizotekezeleka hususani kwa kiwanda cha general tyres
ambacho kilikuwa kikitoa matairi bora kuliko mengine katika nchi za
ukanda wa Afrika Mashariki.
Akijibu swali hilo waziri mwijage amesema
kinachofanyika sasa ni kubadili mitambo ya kiwanda hicho kwa kuwa
iliyokuwepo imechakaa na baada ya muda mfupi kiwanda hicho kitaanza kazi
ili kiweze kuajiri mamia ya vijana wengi.
0 comments:
Post a Comment