Home » » VIGOGO WA IFADI ZIARANI TANZANIA

VIGOGO WA IFADI ZIARANI TANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Ujumbe wa Bodi ya Utendaji ya Shirika la Kimataifa la Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo (Ifad), upo nchini kwa ziara ya siku tano kuanzia jana, kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ya kilimo.
Ujumbe huo wa watu wanane kutoka mataifa ya Uswisi, Finland, Uholanzi, Nigeria, Mexico, Indonesia, China, na Angola pia utafanya mazungumzo na viongozi mbalimbali nchini wakiwamo Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein.
Taarifa ya Ifad kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, ilisema wajumbe hao watafanya tathmini kuhusu ufanisi wa miradi inayodhaminiwa na Ifad kujua imechochea kwa kiasi gani maendeleo ya kilimo nchini. “Ujumbe wa bodi utatembelea miradi inayofadhiliwa na Ifad, Tanzania Bara na Visiwani pia utajadiliana na wanavijiji kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo katika kilimo,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Ifad imewekeza takriban Dola 212 milioni za Marekani (Sh339.2 bilioni) katika miradi mitano inayoendelea ambayo kwa ujumla wake inagharimu Dola 500 milioni za Marekani (Sh800 bilioni). Miradi hiyo inatarajiwa kunufaisha kaya milioni tatu nchini.
Ujumbe huo pia utakutana na Sekretarieti ya Maendeleo ya Kilimo Kusini Tanzania (Sagcot), Idara ya Rais ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), sekta binafsi na washirika wengine wa maendeleo kujadili namna ya kuboresha kilimo cha wakulima wadogowadogo kuwa chenye tija.
Tanzania ni nchi ya pili Mashariki na Kusini mwa Afrika inayopokea msaada mingi ya Ifad katika miradi ya kilimo baada ya Ethiopia.
Ifad imegharimia jumla ya miradi 15 tangu mwaka 1978 yenye thamani ya Dola 769 milioni za Marekani (Sh1.23 trilioni) na kati ya fedha hizo, Dola 360 milioni (Sh576 bilioni) zilitoka moja kwa moja katika mfuko huo.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa