Home » » JK kufungua mkutano wa Mpango wa Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazi‏

JK kufungua mkutano wa Mpango wa Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazi‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Jakaya Kikwete anatarajia kufungua mkutano wa Kanda ya Afrika kuhusu Mpango wa Uendeshaji wa  Shughuli za Serikali kwa uwazi (OGP).

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ikulu inaeleza kuwa mkutano huo wenye kauli mbiu isemayo “Kuimarisha Utawala Bora Unaozingatia Uwajibikaji na Uwazi” utafanyika Mei 20 hadi 21, 2015 katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Aidha, imeeleza kuwa dhumuni la  mkutano huo ni kuleta ufanisi katika utekelezaji wa masuala mbalimbali ya uwajibikaji na utawala wa Serikali ili kutoa mrejesho kwa wananchi pamoja na uwazi kuhusu masuala ya ardhi.

“Kupata uzoefu wa utekelezaji wa OGP kutoka nchi wanachama katika bara la Afrika nan je ya Afrika kama vile taarifa za uwazi zinazoimarisha uwajibikaji” iliongeza taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilisema  kuwa mkutano huo ni wa kwanza kufanyika nchini Tanzania na ni wa pili kwa Kanda ya Afrika ambapo kwa mara ya kwanza  ulifanyika nchini Mombasa nchini Kenya mwaka 2013.

Mkutano huo unatarajiwa kuwa na washiriki 200 kutoka Serikalini, Asasi za kirai, Washirika wa Maendeleo wakiwemo Mawaziri kutoka ndani na nje ya nchi, Makatibu Wakuu, Wakuu wa baadhi ya Taasisi za Serikali, wawakilishi kutoka Nchi wanachana wa OGP kutoka bara la Afrika.

Washiriki wengine ni kutoka nchi za Botswana, Zambia, Uganda, Marekani, Zimbabwe pamoja na washirika wa Maendeleo kutoka Benki ya Dunia, UNDP, UNICEF, UNESCO, MCC, USAID, DFID na JICA.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa