Frank
Mvungi-Maelezo.
Takribani
raia 4792 wa kigeni wamekamatwa kwa kukiuka sheria, Kanuni na Taratibu za
Uhamiaji katika kipindi cha Januari hadi aprili mwaka huu.
Kauli hiyo
imetolewa leo jijini Dar es salam na Kaimu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji Bw. Abass
Irovya wakati wa mkutano na Vyombo vya habari
uliolenga kutoa taarifa ya Operesheni mbalimbali zinazotekelezwa na
Idara hiyo.
Irovya
amesema kuwa Idara hiyo imekuwa ikiendesha Operesheni ondoa uhamiaji haramu
tangu mwezi Desemba mwaka jana na imeonyesha mafanikio ambapo raia 1796 wamefukuzwa nchini kwa kukiuka sheria za uhamiaji.
“Wananchi
walio wengi wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa Idara yetu kutokana na uelewa wao
kuongezeka kwa sababu tunayo programu ya kutoa elimu kwa umma na imeonyesha mafanikio
makubwa” alisisitiza Irovya
Bw. Irovya
aliongeza kuwa waliohukumiwa kifungo ni raia 132 na 383 kesi zao zinaendelea
kwenye mahakama katika Mikoa mbalimbali hapa nchini.
Raia 388
walilipa faini hali iliyochangia kuongeza mapato ya Serikali kutokana na
kukiuka sheria na Kanuni za Uhamiaji hapa nchini.
Kwa upande
mwingine kesi 509 zinaendelea katika mahakama mbalimbali hapa nchini na raia 294 waliachiwa huru kutokana na mahakama kutowatia hatiani.
Idara ya
Uhamiaji ina Vituo takribani 60 katika Mikoa Mbalimbali hapa nchini baadhi
vikiwa katika Mikoa ya Tanga,Lindi,Mtwara,Ruvuma,Katavi,Kigoma,Simiyu ambapo
Idara hiyo imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu athari za raia wa kigeni
wanaoingia nchini bila kufuata sheria na taratibu za Uhamiaji.

0 comments:
Post a Comment