Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA CHADEMA NA WANAHABARI JUU YA KUWAVUA UONGOZI BAADHI YA VIONGOZI

YALIYOJILI KATIKA MKUTANO WA CHADEMA NA WANAHABARI JUU YA KUWAVUA UONGOZI BAADHI YA VIONGOZI

Baada ya mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)  kuwasili alianza kwa kusema kuwa kamati kuu imemteua kamanda Tundu Lissu kuwa mwanasheria mkuu wa chama na pia kamati kuu imefikia maamuzi ya kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa baadhi ya viongozi.
Mwenyekiti akamkaribisha Tundu Lissu kwa ajili  ya kutoa taarifa ya maadhimisho ya kamati kuu kwa niaba yake.
Tundu Lissu alianza kwa kusema kuwa kamati kuu imefanikiwa kupata waraka wa siri wenye mpango wa kukipasua chama chini ya uratibu wa Zitto Kabwe,  Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na mtu mwingine ambaye bado awajafanikiwa kumpata.
Lissu anaendelea kueleza waraka huo uliopewa jina la waraka wa ushindi inavunja  katiba ya chama na wala wahusika awajawahii kuwasilishwa kwenye kikao chochote halali cha chama.
Lissu alieleza kuwa wahusika waliomba kujiuzulu baada ya waraka huo kukamata lakini uongozi wa chama ulikataa kwa vile awakuona sababu ya watu hao kupata nafasi ya kuondoka kwa heshima ambayo awastahili.
Aidha chama hicho kimeagizwa kuwaandikia barua wahusika kuwataka wajieleze kwanini wasivuliwe uanachama kwa kosa kubwa waliofanya.
Mwisho alimaliza kwa kusema waraka huo utasambazwa nchi nzima ili wananchi wausome.

1 comments:

clavery said...

Tunautaka waraka huo tafadhali.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa