Baada ya mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)
kuwasili alianza kwa kusema kuwa kamati kuu imemteua kamanda Tundu
Lissu kuwa mwanasheria mkuu wa chama na pia kamati kuu imefikia maamuzi
ya kuwachukulia hatua za kinidhamu kwa baadhi ya viongozi.
Mwenyekiti akamkaribisha Tundu Lissu kwa ajili ya kutoa taarifa ya maadhimisho ya kamati kuu kwa niaba yake.
Tundu Lissu alianza kwa kusema kuwa kamati kuu imefanikiwa kupata
waraka wa siri wenye mpango wa kukipasua chama chini ya uratibu wa Zitto
Kabwe, Kitila Mkumbo, Samson Mwigamba na mtu mwingine ambaye bado
awajafanikiwa kumpata.
Lissu anaendelea kueleza waraka huo uliopewa jina la waraka wa
ushindi inavunja katiba ya chama na wala wahusika awajawahii
kuwasilishwa kwenye kikao chochote halali cha chama.
Lissu alieleza kuwa wahusika waliomba kujiuzulu baada ya waraka huo
kukamata lakini uongozi wa chama ulikataa kwa vile awakuona sababu ya
watu hao kupata nafasi ya kuondoka kwa heshima ambayo awastahili.
Aidha chama hicho kimeagizwa kuwaandikia barua wahusika kuwataka
wajieleze kwanini wasivuliwe uanachama kwa kosa kubwa waliofanya.
Mwisho alimaliza kwa kusema waraka huo utasambazwa nchi nzima ili wananchi wausome.
1 comments:
Tunautaka waraka huo tafadhali.
Post a Comment