Tanzania Arts Group limefanya
ziara katika ofisi za Tone Multimedia Group ambao ni wamiliki wa blogs za mikoa
na radio ya mtandaoni kwa lengo la kujionea namna kampuni hii inavyofanya kazi
za kidigitali.
Mwenyekiti wa kundi hilo
Manuari Mruma ‘Mr Nzoke’ na wanakikundi wenzake, pamoja na kujionea shughuli za
Tone pia lilionyesha vipande kadhaa vya maigizo na kueleza mipango yake ya
baadae katika kuendeleza sanaa ya filamu na maigizo.
Kundi la Tanzania Arts katika picha ya pamoja walipotembelea ofisi za Tone Multimedia
Mhariri wa habari, Dotto Kahindi (wa pili kushoto) akitoa maelezo kwa wanakundi hao
Mwenyekiti wa kundi hilo
Manuari Mruma ‘Mr Nzoke’ akiuliza jambo
Mwandishi wa habari za burudani, Seki David akifafanua jambo kwa wageni hao
Mmoja wa wanakundi akiigiza kama mtoto yatima anayeteswa na walezi wake
Tanzania Arts Group ni kundi
changa la sanaa linalohitaji michango mingi
kutoka kwa wadau mbalimbali wa sanaa ikiwa ni pamoja na msaada wa
mawazo, ushauri na ushirikiano ili kuboresha kazi yake.
Kwa wale wanaopenda kufanya
kazi na wasanii wa kundi hilo wanaweza kufanya mawasiliano na mwenyekiti wa
kundi hilo Mr. Nzoke kwa simu namba 0658450420 au 0767929474.
0 comments:
Post a Comment