Na Immaculate Makilika –MAELEZO
Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Yusuph Makamba alisema kuwa Rais Magufuli anafanana na Yohana Mbatizaji kwa vile ni kiongozi anayefanyakazi bila kuogopa.
Makamba ametoa kauli hiyo leo kwa njia ya simu katika mahojiano maalum na Mwandishi wa habari hizi.
Makamba alisema kuwa Rais ni kiongozi mchapakazi ambaye hayumbushwi na maneno wala vitisho kwa vile anasema ukweli katika kutekeleza majukumu yake.
“Yohana
Mbatizaji alisema ukweli na hakutikiswa na upepo, hakuogopa macho ya
watu wala hakuwa mtu wa majigambo, kama ilivyoandikwa katika Biblia
Takatifu Marko 6:12, na hivyo ndiyo navyomfananisha Rais wetu Magufuli
na viongozi wote tumuunge mkono” alisema Makamba.
Aidha, kuhusu maika 55 ya Uhuru , alisema kuwa ni vyema Watanzania wakazingatia wito wa uhuru ni kazi, na kwa kuwa Serikali hii imeweka mkazo katika ufanyaji kazi.
Makamba alisema
kuwa katika Awamu hii ya HAPAKAZI TU, inaakisi wito wa Uhuru katika
vipindi mbalimbali kuanzia kipindi cha Uhuru ni kazi na Uhuru na kazi
mara baada ya kupatikana kwa Uhuru na kuwakumbusha watanzania kuulinda Uhuru.
“Ni lazima kuulinda Uhuru kwa gharama yeyote ili amani na mshikamano uendelee kuwepo basi hatuna budii kuepuka lugha zenye maneno ya uchochezi, ukabila na udini” alisema Makamba
mwisho
0 comments:
Post a Comment