Na. Eliphace Marwa – Maelezo.
02/12/2016
Aliyekuwa
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Augustine Mrema
amemfananisha Rais John Pombe Magufuli na Baba wa Taifa Mwl. Julius
Kambarage Nyerere katika utendaji kazi wake.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hii Lyatonga alisema kuwa utendaji kazi wa Rais
Magufuli hautofautiani na ule wa wa Baba wa Taifa kwani wote wanachukia rushwa, ufisadi na kujilimbikizia mali kwa viongozi wa serikali.
“Mwalimu
Nyerere alichukia sana rushwa na alichukua hatua kali sana kwa wala
rushwa wote bila kujali nyadhifa zao au uwezo wao wa kifedha, nakumbuka
kuna waziri wake mmoja alihukumiwa kifungo na viboko baada ya kupatikana
na hatia ya kula rushwa”, alisema Lyatonga.
Aliongeza
kuwa Watumishi wote wa umma, waliohusika na ufisadi walichukuliwa hatua
kali ikiwa ni pamoja na kufungwa jela na kufilisiwa mali zao
nakupelekea kupunguza sana rushwa na ufusadi serikalini.
“Mwalimu
Nyerere alileta Azimio la Arusha ambalo lilizuia viongozi
kujilimbikizia mali na alitenganisha siasa na biashara ambapo wanasiasa
hawakuruhusiwa kufanya biashara na wafanyabiashara hawakuruhusiwa
kushika nafasi za uongozi kitendo ambacho Dkt. Magufuli anafuata nyayo
zake”, alisema Lyatonga.
Mrema
aliongeza kuwa Viongozi wa leo wanapaswa kujifunza kutoka kwa Mwalimu
Nyerere kwani Mwalimu alikuwa muadilifu, hakujilimbikizia mali, na wala
hakuwahi kutumia madaraka yake kwa manufaa yake binafsi ndiyo maana
hata watoto wake walisoma shule ndani ya nchi yetu kwenye shule za kawaida.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment