Christina
Njovu, NEC
Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC imepokea ujumbe
Taasisi ya Tume za Uchaguzi Duniani
(AWEB) uliokuja kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala mbalimbali ya
uendeshaji Uchaguzi.
Ujumbe huo umekuja kujifunza kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) juu ya masuala mbalimbali ya uendeshaji Uchaguzi nchini ikiwemo matumizi
ya vifaa vya kuandikishia wapiga kura.
Mkurugenzi wa Mipango na Oparesheni Bw. Lee Ju-Hwan alisema kuwa yeye na ujumbe wake wamekuja kubadilishana
uzoefu katika technolojia ya Kuandikisha Wapiga Kura.
Ujumbe
huo umekutana na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Bw. Kailima Ramadhani na kufanya
mazungumzo naye ofisini kwake baada ya kukutana na baadhi ya wajumbe wa
Menejimenti ya tume hiyo kutembelea ofisi mbalimbali za Tume hiyo na kujifunza.
Wakiwa
katika kikao na baadhi ya Watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ujumbe huo wa
watu watatu ulijifunza namna mashine ya Biometric Voter Registration (BVR)
inavyofanya kazi na jinsi NEC ilivyoweza kuandikisha Wapiga Kura wengi kwa
kutumia mashine technolojia hiyo na
changamoto zake.
Aidha
ujumbe huo umekuja na aina mpya ya technologia ambayo inauwezo wa kuandikisha
Wapiga Kura, kutuma taarifa za Wapiga katika kanzidata kutoka katika kituo cha kujiandikishia
na kuhakiki Wapiga Kura siku ya Uchaguzi
.
Mashine
hiyo ambayo ni ndogo ukilinganisha na ile BVR ina uwezo wa kutumiwa na mtu
mmoja ambaye ataweza kumuandikisha Mpiga Kura katika hatua zote hadi kupata
kitambulisho cha mpiga Kura na inabebeka kirahisi.
Ujumbe
huo umeongozwa na Mkurugenzi wa Mipango na Operesheni Lee Ju-Hwan, Mtafiti Moon
Jueun na Mtaalamu wa Uchaguzi Park Jae Sumg.
Technologia
hiyo mpya inaweza kurahisisha utendaji kazi katika masuala ya uandikishaji
wapiga Kura, kuhakiki wapiga kura na kutuma taarifa katika kanzi dara.
0 comments:
Post a Comment