Home » » WANAHABARI 10 KUTEMBELEA IRAN

WANAHABARI 10 KUTEMBELEA IRAN

na Mwandishi wetu
WANAHABARI kumi kutoka kwenye vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini wanatarajiwa kwenda nchini Iran kujifunza utamaduni wa nchi hiyo.
Akizungumza na Jukwaa la Habari (TANEF), Ofisa Ubalozi wa Kituo cha Utamaduni wa Iran, Morteza Sabouri, alisema kuwa ubalozi wao umeanzisha mkakati wa kubadilishana uzoefu wa kutangaza utamaduni wa Tanzania na Iran.
“Kwanza tunatarajia kuwapeleka waandishi 10 wa habari katika tamasha la utamaduni linalotarajiwa kufanyika mwaka huu Iran, tunaamini kuwa baada ya kuwapeleka watajifunza mambo mengi ambayo kama wakirejea wasaidia kutangaza utamaduni wetu,” alisema Sabouri.
Afisa ubalozi huyo ambaye yupo katika ziara ya kutembelea redio za hapa nchini ili kuona namna watakavyoweza kubadalishana vipindi vya maendeleo alisema kuwa wana mipango ya kuwa wanaleta vipindi vyao Tanzania.
Naye Meneja wa redio Hits FM, tawi la Dar es Salaam, Rose Ngonyani, alisema kuwa ofisa ubalozi huyo anatarajia kwenda mjini Zanzibar wiki ijayo ikiwa ni mwendelezo wa kutembelea studio za redio hiyo na kuona namna ya kubadilishana vipindi.
Rose alisema kuwa wamepokea maombi ya Iran yenye lengo la kutangaza vipindi vya utamaduni wa nchi ya hiyo na kwamba wapo tayari kuwapatia vipindi wakatangaze.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa