Home »
» Rage aigeuka Yanga kweupe
Rage aigeuka Yanga kweupe
Dar.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage amesema msimamo wa Simba ni
kwamba kukitokea mdhamini katika Ligi Kuu Bara, inapaswa kila klabu
ipewe mgao sawa.
Rage alisema Azam wanakuja kuonyesha Ligi Kuu kwa hiyo sisi tunaomba tupewe mgao sawa na klabu nyingine. Tusiwe wabinafsi.
Kauli hiyo ya Rage inapingana na ile aliyotoa wiki chache zilizopita
aliposema kwamba hawawezi kupewa mgao sawa na klabu nyingine wakati wao
na wapinzani wao Yanga ni timu kubwa na kutangaza kuweka mkakati wa
kuhakikisha wanagomea mkataba huo wa Azam.
Awali, Yanga na
Simba waliungana kutaka walipwe zaidi ya klabu nyingine ambazo kila moja
itapewa Sh100 milioni kutoka kwa Azam TV, itakayokuwa na haki ya
kuonyesha mechi za Ligi Kuu.
Hata hivyo, usiku wa kuamkia jana
Rage alichekelea mamilioini ya Azam na kuwageuka mahasimu wao Yanga
ambao walipanga wote kugomea mkataba huo na badala yake kuukubali ule wa
SuperSports.
Katika sherehe hiyo Simba iliingia mkataba wa
Sh331 milioni na Kampuni ya Azam Media ili kipindi cha Simba TV kiwe
kinaonekana katika televisheni ya Azam (Azam TV).
Katika hafla
Simba walikabidhiwa Sh100 milioni ambazo ni kwa ajili ya udhamini wa
mwaka wa kwanza zilizokabidhiwa kwa Rage. Mwaka wa pili, Simba itapewa
Sh110 milioni na mwaka wa tatu watapokea Sh111 milioni.
“Huu ni mkataba wa aina yake, yaani siku ya kwanza tu tumepewe hundi ya Sh100 milioni,” alitamba Rage.
Rage alisema bajeti ya Simba kwa mwaka ni Sh1.6 bilioni, lakini kiasi
walichokipata kutoka Azam, wakipata na fedha za mauzo ya Emmanuel Okwi
Sh480 milioni pamoja na Sh100 milioni nyingine ambazo watapewa na Azam
Tv za udhamini wa ligi, hiyo itafanya Simba kuwa na akaunti
iliyojitosheleza.
Chanzo: Habari Leo
0 comments:
Post a Comment