Mwenyekiti wa wabunge wa Tanzania Katika Bunge la Afrika Mashariki, 
Mhe. Adam Kimbisa akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa 
habari jijini Dar es Salaam jana. Kushoto ni Katibu wa wabunge wa 
Tanzania katika bunge hilo, Shy-Rose Bhanji, mbunge wa bunge hilo, 
Nderakindo Kessy na kulia ni Mhe. Makongoro Nyerere.
Katibu wa wabunge wa Afrika Mashari kutoka Tanzania, Shy-Rose Bhanji 
akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es 
Salaam. Kulia ni Mhe. Nderakindo Kessy  na Mwenyekiti wa wabunge wa 
Tanzania katika Bunge hilo, Mhe. Adam Kimbisa. 
Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania wakibadilisha 
mawazo baada ya mkutano wao na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam 
jana. Kutoka kushoto ni Katibu wa Wabunge wa Afrika Mashariki kutoka 
Tanzania, Shy-Rose Bhanji, Mwenyekiti, Adam Kimbisa, Nderakindo Kessy na
 Makongoro Nyerere.
Mbunge la Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania Mh. Makongoro 
Nyerere akipeana mkono na Katibu wa wabunge wa Tanzania katika Bunge 
hilo, Mhe. Shy-Rose Bhanji.
DAR ES SALAAM, Tanzania
Bunge la tatu EALA limeridhia Tanzania kupata kikao chake rasmi ambapo 
sasa kikao kitafanyika Dodoma na vikao vingine viwili kufanyika Arusha 
ambayo ni Makao Makuu ya Jumuiya  ya Afrika Mashariki.
Mwenyekiti wa wabunge wa Tanzania, mhe. Adam Kimbisa amesema hayo katika
 mkutano na wabunge watanzania EALA, na waandishi wa habari jijini Dar 
es Salaam, leo.
Mhe. Kimbisa amesema katika ratiba ya vikao vya Bunge la EALA, Tanzania 
pia imepata rasmi kikao kimoja ambapo sasa  kitafanyika mjini Dodoma.
Vile vile amesema kikao hicho kinaweza kufanyika Dar es Salaama au Zanzibar.
Amefafanua kwamba, Bunge limeridhia vikao viwili vifanyike Arusha, 
kimoja kifanyike Tanzania sambamba na nchi zingine wanachama; Kenya, 
Uganda, Rwanda na Burundi kupata kikao kimoja kila nchi kwa mzunguko.
Amesema nchi ambayo itakosa kikao kwa mwaka huu wa fedha 2013/2014, ndio
 itakuwa nchi ya kwanza kupata kikao cha mwaka ujao wa fedha.
Hata hivyo amesema, vikao vikao viwili vya Arusha vitakuwa ni vikao vya 
bajeti na ukaguzi wa mahesabu ambavyo ni vikao muhimu sana katika Bunge.
Mhe. Kimbisa amesema kikubwa wananchi wanachotakiwa kufahamu ni kuwa 
linapokuja suala la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Arusha ni Makao Makuu 
na kwamba haiko Tanzania kwani nchi zote tano ni wadau wa Arusha.
Naye Katibu wa watanzania, Shy-Rose Bhanji amesema ni jambo la kujivunia
 kwamba Tanzania sasa itakuwa na kikao rasmi kwa njia ya mazungumzo. Hii
 ni hatua nzuri vile wananchi pia watapata mwamko wa masuala 
yanayojadiliwa Bungeni.
Hatua ya maridhiano hayo imefuatia mgoghoro ulioibuka miongoni mwa 
wabunge wa EALA kwamba vikao vya Bunge hilo vifanyike Arusha kwa mwaka 
mmoja wa fedha na si kwa mzunguko kama ilivyozoeleka kuanzia Bunge la 
pili.
Wabunge wengi isipokuwa watanzania walitaka vikao viendelee kwa mzunguko nchini Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Arusha.
Vikao vya EALA hadi mwaka wa fedha June 2012/June 2013 vilikuwa vitano 
kwa mwaka. Vikao hivyo vimeongezeka kuwa sita. Vikao hufanyika kila 
baada ya takriban miezi miwili, kwa kipindi cha wiki mbili.
CHANZO: VIJIMAMBO BLOG 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment