MTANGAZAJI wa Kipindi cha Mama Land, kinachorushwa na Runinga ya Clouds ya jijini Dar, Benny Kinyaiya hivi karibuni alikombwa vitu kadhaa kwenye gari lake na vibaka mara baada ya kupaki gari nje ya nyumba yake.
Habari zinapasha kwamba, baada ya kuingia wezi hao walitumia fursa hiyo kuvunja vioo na kuiba redio na vitu vingine.
“Inauma sana kwani kilikuwa ni kitendo kama cha dakika chache tu, yaani kuingia ndani na kutoka tu tayari nimeshaibiwa, natamani hata nimkamate mmoja ili nimuoneshe mfano,” alisema Kinyaiya.
0 comments:
Post a Comment