Home » » Mizani ya nyama kwenye mabucha mingi imechakachuliwa

Mizani ya nyama kwenye mabucha mingi imechakachuliwa

WAKALA wa Vipimo nchini (WMA) anakabiliwa na changamoto mbalimbali katika ukaguzi wa maduka ya nyama (bucha) zikiwamo za wamiliki kutumia mawe yenye uzito pungufu.
Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Meneja Mkaguzi wa WMA, Richard Kadege, alipozungumza na waandishi wa habari na kuzitaja changamoto nyingine kuwa ni kutumia mizani isiyotumika kisheria, kutumia mihuri isiyo na muhuri wa serikali, pamoja na mawe.
Alisema changamoto nyingine ni kuharibu mizani kwa makusudi ili kuwaibia wateja, mfano kutegua pini za mizani, kuwakimbia wakaguzi, kunatisha nyama katika sahani pamoja na kuweka smaku katika mizani.
Meneja huyo pia alisema kufunga uzi kwenye binu upande wa mteja kuelekea chini ya meza na kuwatolea lugha ya matusi na vitisho vya kisu wakaguzi ni changamoto nyingine.
Pamoja na changamoto hizo, Kadege alisema Wakala aliitisha kikao cha wadau wa maduka ya nyama jijini ambapo uamuzi ulikuwa ni kuitisha kikao cha pamoja kati ya wauza nyama, wamiliki na Wizara ya Kazi na Ajira.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa