Kiuswazi
zaidi tunasema, hayawi hayawi sasa yamekuwa, Octoba 18, 2013 shirika la
ndege lenye bei nafuu la fastjet limefanikiwa kuanza safari yake ya
kwanza ya kimataifa kati ya Dar es Salaam na Johannesburg.
Safari
hiyo ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu na watu wengi hatimaye imeanza
rasmi na kufungua milango ya watu wengi kusafiri kati ya Tanzania na
Afrika Kusini kwa gharama nafuu.
Nilikuwa
kwenye safari hiyo ya uzinduzi na mambo yalikuwa hivi; Saa moja na
dakika kumi na tano asubuhi ndo ninaingia uwanja wa ndege wa kimataifa
wa Julius Nyerere na kufanya ukaguzi kabla ya kuingia ndani ya ndege ya
fastjet kutoka Dar es Salaam kwenda Johannesburg Afrika Kusini.
Nikakutana
na abiria wengine ambao nao walikuwa katika safari hiyo ya kwanza, big
up kwao maana wame-experience jambo jipya na jema, kuna hafla fupi ya
uzinduzi wa safari hiyo ilifanyika na abiria wote kupata fursa ya kula
na kunywa pamoja kabla ya kuingia kwenye ndege.
Baada
ya hapo, watu tukapanda zetu ndani ya pipa, na ilipofika saa 3:30
asubuhi ndege ikanyanyuka angani, safari ambayo ilidumu kwa muda wa
masaa matatu na nusu, sawa na dakika 210, hivyo tulifika uwanja wa ndege
wa O.R Tambo, Johannesburg saa 6:00 mchana kwa saa za Afrika kusini.
Safari
kati ya Dar es Salaam na Johannesburg nauli yake ni shilingi 160,000 za
kitanzania bila VAT, na safari zitafanyika mara tatu kwa wiki, yaani
siku za jumatatu, jumatano na ijumaa.
Nisiseme
mengi karibu utazame picha za uzinduzi huo wa safari ya kwanza kabisa
ya kimataifa ya fastjet shirika lenye bei nafuu kabisa.
Mhariri wa habari wa blogszamikoa Dotto Kahindi akiwa na Afisa Masoko wa fastjet, Lucy Mbogoro
Maelekezo ndani ya ndege
Dotto Kahindi akiwa na Millard Ayo
Venance
Commercial manager wa fastjet, Gean Uku
Mike akikata keki
Mike na Lucy Mbogoro wakiweka mambo sawa ili watu tuanze kushambulia keki
Fastjeti kwenye anga ya Tanzania
fastjet ikikata mawingu
Johannesburg kwa juu
fastjet kwenye parking uwanja wa ndege O.R Tambo, Afrika Kusini
Abiria Fina, Dotto na Grace
Abiria wakisubiri kuingia kwenye ndege
Mpiga picha kapigwa picha na mpiga picha akipiga picha
























0 comments:
Post a Comment