Home » » VERY HOT NUUUUZ: Waendesha bodaboda, bajaj wasusia mkutano wa Uhai Tanzania, wadai kuna ubabaishaji

VERY HOT NUUUUZ: Waendesha bodaboda, bajaj wasusia mkutano wa Uhai Tanzania, wadai kuna ubabaishaji


 Mkurugenzi wa UHAI Tanzania Deus Nshekanabo (kushoto) na Aliyejitambulisha kama Katibu wa umoja wa waendesha bajaji, bodaboda Wilaya ya Kinondoni Uwesu Mohamed.

Waendesha bodaboda, bajaj mkoa wa Dar es Salaam wagoma kuhudhuria mkutano ulioandaliwa na Asasi ya Uhai Tanzania wakidai kuwa harufu ya ulaghai na ufisadi inanukia katika asasi hiyo. 

Wakiongea na mtandao huu wamesema hawana imani na Mkurugenzi wa UHAI Tanzania Deus Nshekanabo ambaye ndiye ameandaa mkutano huo kwa waendesha bodaboda na bajaji mkoa wa Dar es Salaam ili kuwapa elimu na maarifa yakuanzisha Benki ya Vijana iitwayo Ajira Vijana Foundation Bank –AVFB uliokuwa umeandaliwa na asasi ya kitaifa ya afya ya umma (UHAI Tanzania) United Health Action Initiatives-UHAI.
 Makamu Mwenyekiti, Rangi

Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Bodaboda na bajaj Afrika Sana, Musdicky Rangi amesema wanachama wake wameshindwa kuhudhuria mkutano huo baada ya kupata taarifa kuwa asasi hiyo imekuwa ikitapeli vijana.

“Vijana wamekataa kuja kwenye mkutano huu kwa kuwa kuna mambo mengi hayajawekwa wazi, hatujui Uhai ni kitu gani, wamesajiliwa ama la, halafu anakuja hapa na gia ya kutumia majina ya marais wastaafu wakidhani tutawaanmini kirahisi” anasema Rangi na kuongeza kuwa:

“Kama kweli anahitaji kufanya mkutano wa kuanzisha benki ya vijana, kwanini wanatuletea watu ambao hata hawaeleweki, tumemuuliza maswali amebaki akijiumauma tu, kuna dalili ya ufisadi na utapeli hapa” 

Awali Asasi hiyo iliandaa mkutano huo ambao ulipangwa kufanyika leo Octoba 14 kwenye ukumbi wa HEKO HALL Sinza Afrika Sana kuanzia saa tatu kamili aubuhi uligonga mwamba baada ya waandaaji kuhusishwa na utapeli.

Pamoja na kutangaza kuwa lengo la mkutano huo kukutana na madereva wa bajaji na bodaboda ili kujadili mambo ya uanzishaji benki ya vijana ni kuwakuza nakuwatoa sekta isiyo rasmi kwenda sekta iliyo rasmi ya biashara mkutano huo uligubikwa na ubabaishaji mwingi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uhai Tanzania Deus Nshekanabo anasema mkutano wa leo ulipanga kuwapata vijana watakaoshiriki kwenye mkutano wa uvumbuzi wa mafanikio ya marais wastaafu uliopangwa kufanyika Octoba 25 mwaka huu kwenye hoteli ya Serana.
 Hotuba ya Rais Kikwete

Lakini jambo kubwa lililowashtua madereva bajaji wachache waliofika kweny ukumbi wa Heko ni ile nakala ya hatuba ya mkutano huo wa tarehe 25 ambayo inaonyesha kuwa mgeni rasmi katika mkutano huo atakuwa ni Rais Jakaya Kikwete, akiambatana na marais wastaafu wote, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, wakuu wote wa mikoa


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa