Home » » TANESCO yapeleka kilio wakazi Bonde Msimbazi

TANESCO yapeleka kilio wakazi Bonde Msimbazi

image
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea na operesheni yake ya kuwakatia umeme watu wanaodaiwa kuhujumu shirika hilo, ambapo safari hii limekata na kuondoa nyaya zote za umeme zinazopeleka nishati hiyo katika eneo lote la Msimbazi bondeni.

 Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Ilala, Ahmed Mningwa, alisema operesheni hiyo niendelevu na haitamuacha mtu yeyote ambaye anatumia umeme isivyo halali.
Alisema kwa wananchi wote wa Jangwani na sehemu zingine katika eneo hilo wafike katika ofisi za shirika hilo wakiwa na nyaraka zao halali tangu walivyoanza taratibu zote za kupata umeme na hadi kufikia hatua ya kupata umeme huo.
"Hii ni operesheni endelevu na haitamwacha mtu yeyote, hakuna mita inayotumia umeme tofauti na ilivyotengenezwa na zaidi ya hapo itakuwa imechezewa na wale wote walioomba umeme kihalali basi wategemee kupata umeme muda mfupi ujao, kwani kila kitu kimekamilika," alisema Mningwa.
Kwa upande wake Mkaguzi Kiongozi wa Shirika hilo Mkoa wa Ilala, Christian Simon, alisema utafiti uliofanywa na shirika hilo katika nyumba 30, nyumba 25 zinatumia umeme bila kulipia na nyumba tano hazina mita kabisa, lakini zinatumia umeme.
Alisema operesheni ipo katika maeneo yote ambapo katika baadhi ya maeneo wananchi wameshindwa kutoa ushirikiano na wakati mwingine kukimbia na kuacha nyumba zao na kwamba kwa muda huu shirika hilo linasaka kila uniti moja inayopotea.
Kwa upande wao baadhi ya wakazi katika eneo hilo walisema kumekuwa na tabia ya watu kujiunganishia umeme kiholela na ni vyema shirika hilo likawakamata watu hao na kuwachukulia hatua za kisheria

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa