Home » » Mwili wa Balozi Kazaura kuwasili nchini leo

Mwili wa Balozi Kazaura kuwasili nchini leo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Balozi Fulgence Kazaura (74), unatarajiwa kuwasili nchini leo ukitokea Chennai, India alikokwenda kwa matibabu ya saratani.
Makamu Mkuu wa Chuo cha UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala alisema jana kuwa, mwili huo utawasili alasiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates na kesho kutafanyika misa ya kumwombea katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Peter, Oysterbay kuanzia saa 7.00 mchana.
Profesa Mukandala alisema keshokutwa watatoa heshima za mwisho na kutakuwa na sherehe ya kumuaga katika Ukumbi wa Nkurumah ulioko UDSM kuanzia saa 8.00 mchana.
Balozi Kazaura alifariki Jumamosi iliyopita nchini India.
Alisema Ijumaa asubuhi, mwili wa Balozi Kazaura utasafirishwa kwenda kijijini kwao Kijumo Misenyi Mkoa wa Kagera kwa mazishi yatakayofanyika Jumamosi.
Marehemu aliwahi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa zaidi ya muongo mmoja na mkuu wa chuo hicho kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi mauti yalipomfika.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa