Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Jamal Salum (12), mtoto ambaye aliuawa na
Mohamed Said (36) ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Awali na Madrasa ya Al
Nur Al eneo la Mbagala Charambe Foma, inadaiwa alitobolewa macho kabla
ya kuchinjwa na mtuhumiwa huyo.
Akizungumza nyumbani kwake eneo hilo, Dar es
Salaam jana, baba wa mtoto huyo, Salum Ally alikanusha mtoto huyo kuwa
mwanafunzi katika madrasa ya mtuhumiwa.
Ally alisema siku ya tukio akiwa anarudi kazini
saa 11 jioni, alipopita eneo hilo la madrasa aliona umati wa watu
umezunguka eneo hilo na alishangaa kabla ya kuendelea na safari yake.
Alisema baada ya kufika jirani na nyumbani kwake,
alipishana na mkewe akilia huku akikimbilia eneo la tukio, akipiga
kelele kuwa mtoto wao Jamal kachinjwa.
Mama wa marehemu, Halima Selemani alisema siku ya
tukio, marehemu baada ya kujaladia madaftari yake na mwenzake aitwaye
Ramadhani waliondoka akimtaka amsindikize kwa mjomba wake eneo la jirani
na hapo akachukue kalamu.
Alisema rafiki yake alimhimiza mwenzake waondoke,
huku yeye akiwa ametangulia ndipo mwalimu huyo alipomshika mkono
marehemu na kuingia nae ndani na mwenzake alirudi na kukuta ameshikwa
mkono na ndipo alipoanza kumsihi amwachie.
“Alimsihi sana amwachie kwani hajui kosa lake,
lakini mwalimu huyo hakumsikiliza badala yake akaanza kumchoma kwa kisu
machoni na usoni,” alisema.
Mtoto huyo alizidi kumwombea mwenzake, lakini akiwa hajui lolote alimshuhudia mwalimu huyo akimchinja mwenzake.
Mwili wa mtoto huyo ulizikwa juzi makaburi ya kwa
Mbiku, wakati mwalimu huyo akizikwa kwao Kisiju Pwani. Baadhi ya
majirani walidai ndugu za marehemu waliwasilisha cheti polisi mwaka 2007
kuwa aliugua ugonjwa wa akili.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema alifika
nyumbani kwa marehemu Jamal na kuwataka ndugu kuwa na subira katika
kipindi hiki kigumu cha majonzi na kuiasa jamii kutowaficha watu ambao
wana matatizo hususan yale ya akili.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment