Home » » Sekretarieti ya Maadili kuhakiki viongozi 300

Sekretarieti ya Maadili kuhakiki viongozi 300

Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, inatarajia kuchunguza kwa kuzifanyia uhakiki mali za viongozi 300 katika mwaka wa fedha wa 2013/14.
Lengo likiwa ni kutathmini matamko ya rasilimali na madeni yaliyowasilishwa.
Akizungumza hivi karibuni, Kamishna wa Sekretarieti hiyo, Jaji mstaafu Salome Kaganda aliwaeleza wajumbe wa Kamati ya Katiba na Sheria kuwa, wanatarajia kuanza kazi hiyo Machi mwaka huu baada ya kupokea fedha zilizotengwa kwa kazi hiyo.
“Baadhi ya matamko hayatolewi kwa ukamilifu, kwa mfano kutotaja thamani halisi ya mali hizo, wala sehemu zilipo na jinsi zilivyopatikana na kusita kutaja namba za akaunti za benki na kiwango cha fedha kilichopo,” alisema Jaji Kaganda na kuongeza:
“Pia, kushindwa kutaja mali za mke au mume na watoto walio chini ya miaka 18.”
Jaji Kaganda alisema kumekuwa na changamoto kubwa kwenye ujazaji matamko, viongozi wengi wamekuwa wakichelewa ku wakilisha kama inavyotakiwa Desemba 31 kila mwaka.
“Desemba viongozi wa siasa waliorejesha matamko walikuwa 3,081 sawa na asilimia 76 ya 4,971, wakati viongozi wa utumishi wa umma waliorejesha ni 5,319 kati ya 8,148, hivyo hali ya urejeshaji ilikuwa ni mbaya kutokana na viongozi wengi kutokamilisha hasa watumishi,” alisema.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa