Home » » TATHMINI YA UZIMAJI WAMITAMBO YA ANOLOJAI KUELEKEA DIJITALI YATOLEWA LEO KWA MIKOA SABA

TATHMINI YA UZIMAJI WAMITAMBO YA ANOLOJAI KUELEKEA DIJITALI YATOLEWA LEO KWA MIKOA SABA

 Mkurugenzi wa mamlaka ya mawasiliano (TCRA) Profesa John Nkomo

 Kutoka kulia ni Pro.Nerey Mvungi katikati ni Dr.francis sichona mtaalamu wa Takwimu kushoto ni Mr.F.M Ishengoma mtaalam wa Habari na mawasiliano
 waandishi wa habari wakiwa katika mkutano wa tathimini katika jengo la (TCRA)
 Mtaalam wamawasiliana ya ki electronic Pro.Nerey mvungi
 kaim naibu mkurugenzi Endrew kisaka kulia akiwasambambana 
 Meneja wa mawasiliano (TCRA) Innocent mungi
 Habbi Gunze mkurugenzi wa utangazaji (TCRA)

 Endrew kisaka kaim naibu mkurugenzi utangazaji



Tathimini ya uzimwaji wa mitambo katika kuelekea dijitali na mamlaka ya mawasiliano Tanzania umekamilika ambapo (TCRA) iliweza kuunda jopo la watu watatu katika kufanikisa tathimini hiyo ambao ni wataalamu toka chuo kikuu ,ambapo tathimini hiyo imejengwa katika maeneo makuu matatu .
Eneo la kwanza likiwa ni Tathmini ya utendaji na utoaji huduma za utangazaji kwenye mfumo wa kidijiti ikiwa ni pamoja na usimikaji wa miundo mbinu ya kidijiti,na eneo la pili ni katika Tathmini ya kuangalia jinsi Mamlaka ya Mawasiliano ilivyokuwa imejizatiti kuandaa na kusimamia zoezi zima la uhamaji toka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda kidijiti, eneo la tatu ni watumiaji wa huduma za utangazaji walivyopokea mabadiliko hayo na changamoto zilizopo na eneo la nne na mwisho ni zoezi zima la uzimaji mitambo lilivyoendeshwa.

Jopo hilo lilieleza Mambo ambayo walizingatia katika uzimaji uzimaji wa mitambo kwa awamu ya kwanza katika mikoa saba moja wali hakikisha kuwepo kwa idadi ya soko la visimbuzi kabla mitambo haijazimwa,idadi ya watu walio weza kununua ,elimu kwa wadau wakati wa mchakato wa uzimaji mitambo,ubora wa visimbuzi na upokeaji matangazo

Vivyohivyo jopo hilo lili ainisha njia iliyo tumika katika kufanya tathimini kuwa ni ile njia inayo tumika kimataifa  kuendesha mazoezi kama haya ijulikanayo kama “Sampling Approach” ambapo takwimu hukusanywa kwa kuzingatia uwiano wa kaya zilizopo kwenye eneo husika, jinsia, umri, elimu na kazi za kumuingizia kipato mtu anayehojiwa, Makundi mabalimbali yanayohusika kwenye mchakato huu wa uhamaji kutoka mfumo wa analojia kwenda dijitali yalihojiwa kwa kupitia dodoso maalumu lililoandaliwa na maoni yao yalikusanywa

Baada ya jopo la wataalamu wa Chuo Kikuu kukaa na kufanya tathimini waliamua kutoa matokeo ya tathimini hiyo kama ifuatavyo
1.    Katika utendaji na utoaji huduma za utangazaji katika mfumo wa kidijitali na USIMIKAJI WA MIUNDO MBINU YA KIDIJTI.

(a)   Asilimia 89% ya kaya za watumiaji (consumers) walikuwa wakitumia huduma ya matangazo kwa mfumo wa kidijiti mara baada ya uzimaji wa mitambo ya analojia kwenye miji saba ambayo tathmini ilikuwa ikifanyika

(b)   Asilimia 11% ya kaya za watumiaji hawakuweza kupokea matangazo ya kidijiti kwa sababu mbalimbali kama ifuatavyo:-

-       5.5% hawakununua visimbuizi

-       0.1% ya Kaya, walisema visimbuzi vilikuwa havipatikani

-    3.2% ya Kaya, walishindwa kunua visimbuzi sababu ya bei kuwa juu

-       0.2% ya Kaya visimbuzi vyao vilikuwa vibovu

-     0.3% ya Kaya, visimbuzi havikuweza kupokea matangazo ya kidijiti kwa sababu ya mawimbi hayapatikani kwa ubora zaidi (Poor signal reception)

-       0.9% ya Kaya Luninga (TV screen) zilikuwa mbovu

-       0.7% ya Kaya hawakuwa na umeme


2.   UTAYARI WA MAMLAKA YA MAWASILIANO KUANDAA NA KUSIMAMIA ZOEZI ZIMA LA UHAMAJI TOKA UTANGAZAJI WA MFUMO WA ANALOJIA KWENDA KIDIJITI

- Jopo la wataalamu lililokuwa likiendesha tathmini hii liliweza kuthibitisha kuwepo kwa baadhi ya nyaraka kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ikiwa ni Kuwepo kwa kamati ya Kiufundi inayoundwa na wadau mbalimbali, dira madhubuti inayoonyesha mambo muhimu ya kutekelezwa, sheria na kanuni zinazosimamia zoezi la uhamaji toka analoja kwenda kidijiti,
   Vilevile Jopo la wataalamu liliweza kuthibitisha mambo yafuatayo:-
Muundo bora wa leseni unaozingatia utoaji huduma za matangazo ya kidijiti, Utaratibu mzuri wa ushindani kwa njia ya wazi uliotumika kuwapata “Multiplex Operators” (wajenga Miundombinu na Wsambazaji wa matangazo), Utaratibu mzuri wa ushindani kwa njia ya wazi uliotumika kuwapata “Multiplex Operators” (wajenga Miundombinu na Wsambazaji wa matangazo) na mengine mengi

3.   MATOKEO YA TATHMINI KUHUSU UPATIKANAJI WA VISIMBUZI NA ELIMU KWA UMMA
Tathmini imeonyesha kuwa kati ya kaya zote zilizohojiwa kwenye miji saba, ni 0.1% ya kaya zilizodai uhaba wa visimbuzi wakati wa zoezi zima la uzimaji mitambo ya analojia
4.   ZOEZI LA UZIMAJI MITAMBO YA ANALOJIA
Ilifahamika kuwa zoezi la uzimaji mitambo ya analojia lilifanyika kwenye awamu nne ambapo kila awamu ilitoa nafasi ya mwezi mmoja. Jopo la wataalam limeridhika na utaratibu huu, ambao unatoa nafasi kubwa ya kutathmini matatizo yanayojitokeza kwenye awamu ya kwanza kabla ya kwenda kwenye awamu nyingine. Vilevile ulitoa fursa ya kuhakikisha kuwa eneo linalofuata linakuwa na visimbuzi vya kutosha na elimu kwa umma inatolewa kikamilifu kwa kutumia Radio na Televissheni za eneo husika.
5.   WATENGENEZAJI NA WASAMBAZAJI MAUDHUI (CONTENT SERVICE PROVIDERS)
65% ya watengenezaji na wasambazaji wa maudhui walikuwa wamejiunga na mfumo wa kidijiti kabla ya uzimaji wa mitambo ya analojia.
Sababu kubwa ya vituo vingine kutojiunga na mfumo huu kwa wakati ilikuwa ni sababu za kimazoea kwamba huenda mitambo isingezimwa kwa wakati uliopangwa. Mpaka sasa vituo vyote vilivyopo Dar es Salaam vimeshajiunga na mfumo huu kasoro kituo kimoja.
6.   MAJUMUISHO
Jopo la wataalam limeridhika kuwa watazamaji wengi waliokuwa kwenye mfumo wa analojia walijiunga kwenye mfumo wa kidijiti. 11% tu ndio ambao hawakuweza kujiunga kwa sababu mbalimbali kama nilizoelezea mwanzoni. Idadi hiyo inaweza kuwa imepungua kwa vile watu wamekua wakiendelea kununua visimbuzi,

Kutokana na matokeo ya tathmini iliyofanyika serikali inashauriwa iendelee na zoezi la uzimaji mitambo ya analojia sehemu zilizobakia. Jopo limeridhika na uandaaaji na usimamizi wa zoezi hili na kwamba kasoro zilizojitokeza ni sababu ya hofu ya mabadiliko na uzoefu wa walaji kwenye matumizi ya visimbuzi. Vilevile kuna faida nyingi za mfumo wa kidijiti ambazo watoa huduma wanatakiwa kuzitumia ili kuchochea ukuaji wa uchumi nchini.

Serikali inashauriwa kutoa punguzo la kodi kwa visimbuzi ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kununua visimbuzi na kupata habari kwa njia ya Luninga 


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa