MAHAKAMA
Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Aprili 17 mwaka huu, itatoa uamuzi wa
kuifuta au kuendelea na kesi ya kikatiba inayomkabili Waziri Mkuu, Bw.
Mizengo Pinda pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).
Kesi hiyo
ilikuja mahakamani hapo jana ambapo juzi, Naibu Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, George Masaju, aliomba kufutwa kwa kesi hiyo ambayo
imefunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha
Wanasheria wa Tanganyika (TLS).
Katika kesi hiyo namba 24 ya mwaka
2013, LHRC na TLS, wanadai Bw. Pinda alivunja Katiba kutokana na kauli
aliyoitoa bungeni Mjini Dodoma, kuhusu Polisi kuwapiga raia ambao
watakaidi amri.
Hata hivyo, AG ambaye aliunganishwa katika kesi
hiyo, waliweka pingamizi la awali akidai walalamikaji na watu
walioorodheshwa katika kesi hiyo hawana mamlaka kisheria ya kumfungulia
kesi.
Awali, Masaju alisema, sheria inamlinda Waziri Mkuu
kutoshtakiwa wala kuhojiwa na chombo chochote juu ya kauli aliyoitoa
bungeni; hivyo kesi hiyo ni batili na iko mahakamani isivyo halali.
Alisema
kufunguliwa kwa kesi hiyo ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano
ya mwaka 1977, Sheria ya Mamlaka, Kinga na Haki za Wabunge ya mwaka
1988.
Akifafanua hoja hiyo, Masaju alisema Bw. Pinda analindwa na
Katiba
Ibara ya 100 (1) na (2) inayosema, "kutakuwa na uhuru wa mawazo na
majadiliano bungeni, ambao hautavunjwa wala kuhojiwa na chombo chochote
au katika mahakama yoyote nchini.
Ibara ya pili inasema "mbunge
yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kwa jambo
lolote alilolisema, alilolitenda au alililoliwasilisha bungeni kwa njia
ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo".
Aliongeza kuwa, msingi wa shauri hili unatokana na jambo lililosemwa bungeni na mmoja wa wabunge wakati wa shughuli za bunge.
Kesi hiyo ipo chini ya jopo la majaji watatu ambao ni Jaji Kiongozi Fakh Jundu, Augustino Mwarija na Dkt. Fauz Twaib.
Chanzo;majira
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment